Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia: Polisi jipangeni kwa uchaguzi 2024, 2025
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia: Polisi jipangeni kwa uchaguzi 2024, 2025

Spread the love

RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amelitaka Jeshi la Polisi nchini kujipanga katika kuhakikisha Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu wa 2025, zinafanyika kwa amani bila kuigawa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa maafisa wakuu waandamizi wa Jeshi la Polisi, leo tarehe 4 Septemba 2023, jijini Dar es Salaam, Rais Samia amesema Serikali yake inakwenda kulitafutia fedha kiasi cha Sh. 125 bilioni, ili kuliwezesha kutekeleza majukumu  yake katika kipindi hicho.

“Mwakani tuna uchaguzi wa Serikali za Mitaa, nataka jeshi liwe makini kwelikweli huko katika maeneo mbalimbali, kusimamia haki itendeke, kusimamia usalama katika chaguzi zile, kuhakikisha zinakwenda kwa njia ya usalama,”

“ IGP nimemwambia hilo akaniletea bajeti ya karibu Sh. 125 bilioni ambayo nakwenda kuipekua na ikiwezekana niipate yote ili zile changamoto ziondoke muweze kufanya kazi zenu vizuri,” amesema Rais Samia.

Rais Samia amesema ulinzi na usalama wa Tanzania unalitegemea Jeshi la Polisi “nasema kila siku Tanzania yetu ni moja tu hakuna tena Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulimwenguni, tukiweka vizuri ni sisi watanzania, tukiipasua pasua ni sisi watanzania.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!