UTOAJI huduma za Afya katika Hospitali Kuu ya Musoma Vijijini, mkoani Mara, umezinduliwa rasmi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara…(endelea).
Taraifa ya uzinduzi huo uliofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dk. Khalifan Haule, imetolewa hivi karibuni na Ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo.
Hospitali hiyo ina majengo muhimu tisa. Majengo mengine sita yanaendelea kujenga ikiwemo la kufua.
“Hospitali hii yenye kutoa huduma za afya kwa kiwango cha hadhi ya Hospitali ya Wilaya, hadi sasa Serikali imeshatoa Sh. 3.49 bilioni kwa ajili ya Ujenzi na Sh. 600 milioni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na dawa,” imesema taarifa.
Taarifa hiyo imesema hospitali ina vifaa vya kisasa, vikiwemo Digital x-rays, Ultrasound na mitambi ya kutengeneza Oxygen.
Leave a comment