Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mkutano maandalizi ya uvamizi kijeshi Niger waahirishwa
Kimataifa

Mkutano maandalizi ya uvamizi kijeshi Niger waahirishwa

Spread the love

Mataifa ya Afrika ya Magharibi yamesitisha mkutano muhimu wa kijeshi juu ya mzozo wa Niger ikiwa ni siku moja baada ya kusema maazimio ya mkutano huo yangelituma kuandaa kikosi cha kumrejesha madarakani kiongozi wa nchi hiyo aliyepinduliwa, Mohamed Bazoum.

Wakuu wa majeshi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Uchumi ya Afrika Magharibi (ECOWAS) walikuwa wakutane leo Jumamosi katika mji mkuu wa Ghana, Accra, lakini jioni ya jana Ijumaa kulitolewa tamko la kuuakhirisha mkutano huo kwa muda usiojulikana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Vyanzo hivyo vilisema mkutano huo ulikuwa umeandaliwa ili kuwaeleza viongozi wa ECOWAS juu ya njia bora zaidi za kuunda na kutuma kikosi hicho cha dharura nchini  Niger.

Bado ECOWAS haijafafanua kwa undani kuhusu kikosi hicho wala ratiba ya hatua zake, huku viongozi wake wakisisitiza kuwa bado wanataka suluhisho la amani.

Akhirisho la mkutano huo lilitangazwa wakati maelfu ya wananchi wa Niger wakikusanyika kuunga mkono jeshi lao mbele ya kituo kimoja cha jeshi la Ufaransa jana Ijumaa.

Mkoloni huyo wa zamani ana wanajeshi zaidi ya 1,500 wanaoshiriki kile kinachoitwa “vita dhidi ya makundi ya kigaidi” kwenye taifa hilo la Ukanda wa Sahel.

Tangu mwaka 1990, ECOWAS yenye wanachama 15 imewahi kuingilia kijeshi kwenye mataifa sita miongoni mwa wanachama wake nyakati za vita vya wenyewe kwa wenyewe, uasi ama mkwamo wa kisiasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!