Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko THRDC yalia ukata wasaidizi wa kisheria, yataka wafike gerezani
Habari Mchanganyiko

THRDC yalia ukata wasaidizi wa kisheria, yataka wafike gerezani

Spread the love

MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), imesema kuna uhaba wa watu wanaotoa msaada wa kisheria, kitendo kinachopelekea wananchi kukosa haki ya kufikia vyombo vya kisheria ili kupata haki zao. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumatatu, jijini Dar es Salaam, katika semina ya siku mbili (tarehe 7 hadi 8, Agosti 2023) kuwajengea uwezo watoa huduma ya msaada wa kisheria 60, kutoka mikoa ya Tanga, Pwani na Dar es Salaam.

Mratibu wa THRDC, Onesmo Olengurumwa, amesema Tanzania Ina wasaidizi wa kisheria 5,000 ambao hawatoshi kuwafikia wananchi zaidi ya milioni 60, hususan wa maeneo ya vijijini.

Mbali na uhitaji mkubwa wa wasaidizi hao katika maeneo ya vijijini, Olengurumwa amesema Kuna haja kubwa ya watoa huduma za msaada wa kisheria kuwepo katika magereza yote nchini

“Tumezunguka huko tumeona Kuna haja ya magereza kuwa na watoa msaada wa kisheria, pia tunataka maeneo yote ambayo msaada wa kisheria unahitajika Watanzania wasiikosw huduma hiyo. Watanzania tuko zaidi ya milioni 60, ukitoa watoto nusu yake wanahitaji huduma hii lakini watoaji wako 5,000 na vijiji tunavyo zaidi ya 14,000 utakuta vijiji zaidi ya 7,000 hawana wasaidizi,” amesema Olengurumwa.

Akizungumzia semina hiyo, Olengurumwa amesema wameiratibu ili kuunga mkono Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Samia (Samia Legal Aid Campaign), inayoendelea nchi nzima.

“Tumeona mafunzo haya ni fursa kwa Watetezi lakini kuunga mkono kampeni ya Samia Legal Aid, sababu nyie wasaidizi wa kisheria ndiyo watekelezaji hivyo lazima tuwajengee uwezo kuhakikisha Taasisi za msaada zinakuwa zaidi,” amesema Olengurumwa.

Olengurumwa amesema “hii ni dhana mpya sababu mwanzo tulikuwa na mafunzo ya  elimu kwa wanasheria, sisi tukaja na majaji na Sasa watoa msaada wa kisheria.

“Tunafanya hivi sababu elimu haina mwisho hata profesa anaendelea kuwa darasani kwa kuwa Kila wakati standard zinabadikika, sheria zinatungwa mpya na mazingira yanabadilika hivyo muendelezo wa elimu ni jambo la msingi itasaidia kuwa na Watetezi wenye uwezo wa kuwawezesha Watanzania kulinda haki za binadamu.

Naibu Mkuu wa Shule ya Sheria, Dk. Clement Mashamba, amesema wameanzisha kozi ya huduma ya msaada wa kisheria ili kuongeza umahiri kwa wanaoitoa.

“Mafunzo Maalum ya umahiri kwa wasaidizi wa Kisheria ni miongoni mwa malengo ya sheria yetu ya msaada wa Kisheria, kulikuwa na takwa lazima wapewe mafunzo na tumeanza na mafunzo ngazi ya chetu na baada ya muda tutaanza diploma mpaka tupate ithibati,” amesema Dk. Mashamba na kuongeza:

Wale wasaidizi ambao hawajapata masomo Maalum mnaweza kutumika fursa hiyo dirisha la usajili limeshafunguliwa. Haya ni mafunzo muhimu sababu yanamuandaa mwanafunzi kwenda kutoa huduma bora.”

Mwenyekiti wa Kamati ya Msaada wa Kisheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Veronica Buchumi, amesema mafunzo hayo ni muhimu kwa kuwa yatasaidia wahusika kutoa huduma bora kwa wananchi.

“Dk. Mashamba amesema mafunzo haya ni ya muhimu sana, Sasa huduma za msaada tunazotoa kitu Cha msingi sana sababu wakati mwingine unaweza kusema tunawpaa msaada, lakini ubora ni kitu Cha msingi,” amesema Dk. Buchumi na kuongeza:

“Mafunzo haya yanalenga kuboresha huduma huduma tunazotoa Kwa Watanzania ambao hawaweI kukidhi gharama za mawakili.Wote wamekuja Kwa Nia ya kukuza ujuzi, kujifunza kanuni na tarativu zitakazosaidia kuboresha huduma ya msaada wa Kisheria.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!