Monday , 20 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kamati za Bunge mguu sawa Bunge likianza 29 Agosti
Habari za Siasa

Kamati za Bunge mguu sawa Bunge likianza 29 Agosti

Spread the love

Bunge la Tanzania limesema, vikao vya kawaida vya Kamati za Kudumu za Bunge vitaanza kufanyika Jumatatu tarehe 14 hadi 25 Agosti 2023 Jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya  Mkutano wa 12 wa Bunge utakaonza  tarehe 29 Agosti 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea)

Taarifa kwa umma iliyotolewa na Ofisi ya Bunge leo Jumapili na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa imesema Kamati tano zitatangulia kuanza vikao.

Imesema nne kati ya hizo zitaanza vikao tarehe 7 Agosti 2023 na Kamati moja ya Bajeti itaanza tarehe 10 Agosti 2023.

Imefafanua kuwa shughuli za kamati katika kipindi hicho zitakuwa ni: -Uchambuzi wa Miswada miwili ya Sheria utakaofanywa na Kamati mbili: Kamati ya Utawala, Katiba na Sheria na Kamati ya Bajeti;

Pili ni uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa wakati wa Mkutano wa Kumi na Moja wa Bunge na tatu ni chambuzi wa Taarifa za Hesabu zilizokaguliwa na CAG kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni 2022

Nne ni uchambuzi wa Taarifa za Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa lengo la kuliwezesha Bunge kufuatilia ufanisi na tija kwa Mitaji ya Serikali kwenye mashirika mbalimbali na taasisi; na mwisho ni uchambuzi wa Taarifa za Utendaji za Wizara kwa lengo la kuliwezesha Bunge kutekeleza jukumu la kuisimamia na kuishauri Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!