Monday , 20 May 2024
Home Habari Mchanganyiko RC Dodoma: Nane nane iwe na tija kwa wakulima, wafugaji
Habari Mchanganyiko

RC Dodoma: Nane nane iwe na tija kwa wakulima, wafugaji

Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dodoma, Rosemary Senyamule amesema maonesho ya wakulima ya nane nane yanatakiwa kulenga zaidi kutoa elimu kwa wakulima ili kilimo kiwe chenye tija badala ya kuwa ya kujikimu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Aidha, ameeleza kuwa katika kuelekea sherehe za maadhimisho ya Maonesho ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi nchini ambayo hufanyika kila mwaka nchini kuanzia tarehe 1 Agosti na kufikia kilele tarehe 8 Agosti, kwa Kanda ya Kati imejipanga kuja na mbinu za kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 31 Julai 2023, Senyamule amesema utafiti unaonesha mikoa wa Dodoma na Singida imeendelea kuathiriwa na mabadiliko ya tabia nchi.

Amesema hali hiyo imeathiri uzalishaji wa mazao ya kilimo mifugo na uvuvi, hivyo uongozi wa mikoa hiyo umedhamiria kusambaza mbinu za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na uharibifu wa mazingira.

Ametaja mbinu hizo kuwa ni pamoja kuhifadhi maji na udongo mashambani ikijumuisha matumizi ya makingamaji, kilimo cha mbegu tisa na jembe la mzambia, kuzalisha mazao yanayotumia maji kwa ufanisi kama vile mtama na alizeti).

Pia uzalishaji wa malisho kwa ajili ya mifugo, uhifadhi ya misitu na upandaji wa miti, matumizi ya nishati mbadala (Jua, umeme na gesi) kwa ajili ya kupikia.

“Tutajikita zaidi kusambaza teknolojia za kisasa katika kilimo na ufugaji bora ambapo taasisi za utafiti za kilimo, mifugo na uvuvi zitashiriki maonesho hayo kuonesha teknolojia mbalimbali zilizozalishwa kwenye vituo vya utafiti na kuwawezesha wakulima kunufaika na elimu ya uzalishaji bora,” amesema Senyamule.

Aidha, amesema katika maonesho hayo kutakuwa na matukio muhimu ikiwemo kongamano la tasnia ya alizeti, mtama, siku maalumu ya uhamasishaji uzalishaji kuku wa kienyeji pamoja na tamasha la mashindano ya nyama choma.

Amesema kauli mbiu ya maonesho ya mwaka huu kitaifa ni “Vijana na Wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula” wakati kikanda ni “Kilimo ni Biashara, Biashara ni Uwekezaji.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Elimu ya utunzaji wa mazingira ipewe kipaumbele kwa watoto

Spread the love  JAMII imetakiwa kuwajengea Watoto tabia ya utunzaji wa mazingira...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Watumishi 85,471 walioenguliwa kipindi cha JPM wapandishwa vyeo

Spread the loveSERIKALI imesema kuanzia mwaka wa fedha 2021/2022 hadi sasa jumla...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

error: Content is protected !!