Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko NGOs zabisha hodi kwa Rais Samia
Habari Mchanganyiko

NGOs zabisha hodi kwa Rais Samia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

MASHIRIKA Yasiyo ya Kiserikali (NGO’s) yameomba kuonana na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ili kumkabidhi changamoto zao zilizoshindwa kutatuliwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Wito huo umetolewa katika Jukwaa la Mwaka la NGO’s kwa 2023, linalofanyika jijini Dar es Salaam, kuanzisha leo Ijumaa hadi kesho tarehe 29 Julai mwaka hii.

Miongoni mwa changamoto zinazolalamikiwa na mashirika hayo, ni kutozwa kodi kama taasisi zinazofanya biashara, kuikosa hadhi ya mashirika yanayotoa msaada na kukwama kupata namba za mlipa kodi (TIN number).

Akizungumza katika mjadala huo, Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Usawa wa Kijinsia Tanzania (SUKITA), Msafiri Mwajuma Mariam, amedai changamoto wanazokutana nazo ni kutozwa kodi kubwa, kulazimishwa kuzuia Kodi ya majengo kitendo kinachozuia mgogoro baina Yao na wamiliki wa nyumba wanazopanga.

“Changamoto nyingine tukiomba misamaha ya kodi tunachelewa kupata, wako wengine wameiomba mpaka leo hawajapewa. TRA umsitulazimishe kumfikia mama wakati ninyi mnaweza. Mnatushawishi kumtafuta Rais Samia ili atutatulie shida zetu,” amesema Msafiri.

Naye Mgonja, ameshauri sheria inayosimamia NGO’s, irekebishwe  ili mashirika yanaposajiliwa yapatiwe hadhi ya kutoa misaada, badala ya utaratibu uliopo Sasa wa kusubiri miaka mitatu baada ya kaunzishwa.

Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Onesmo Olengurumwa ameitaka TRA isitoze Kodi fedha ambazo NGO’s zinapokea kutokana na michango ya matembezi ya hiari, kwa kuwa ni fedha za ufadhili.

“Fedha za matembezi ya hiari huo ni mchango kama ruzuku nyingine, inaingia kwenye Shirika kama ruzuku. Pia, changamoto nyingine inavyopaswa kutatuliwa ni NGO’s kupata charitable status, inabidi itatuliwe,” amesema Olengurumwa.

Pia, Olengurumwa ameiomba Serikali itoe msamaha wa jumla kwa NGO’s, pamoja na kuondoa takwa la mashirika yasiyopata fedha za miradi, kuwasilisha taarifa za Mapato na matumizi kila mwezi.

Katika hatua nyingine, wadau hao wameitaka TRA kushirikiana na NGO’s ili wajifunze namna zinavyofanya kazi, kitendo kitakachoondoa migongano baina ya pande zote mbili.

Kwa upande wake Msajili wa NGO’s, Vicky Mayao, amezitaka NGO’s kuunda kamati Maalum itakayokusanya malalamiko yao ya kikodi kwa ajili ya kufikisha TRA ili uafanyiwe kazi.

“Kuna kamati ndogo ya kikodi ilianzishea, nasema warudi mezani sababu sheria za kodi zipo hatuwezi kuzibadilisha hapa, hata tunavyomtaka kamishna hawezi kuja hapa natamani turudi kwenye kamati ya Majadiliano,” amesema Mayao.

Kufuatia malalamiko hayo, Afisa kutoka TRA aliyejitambulisha kwa jina la Mario, amesema changamoto zote zitawasilishwa kwa Kamishna Mkuu wa TRA, kwa ajili ya kufanyiwa kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!