Friday , 17 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Mganga mfawidhi mbaroni madai wizi wa dawa, vifaa tiba
AfyaTangulizi

Mganga mfawidhi mbaroni madai wizi wa dawa, vifaa tiba

Spread the love

Jeshi la Polisi mkoa wa Songwe linamshikilia mtumishi mmoja aitwaye Rioba Nyamos (34) ambaye ni Mganga mfawidhi wa Zahanati ya Kijiji Cha Iporoto akiwa anaiba dawa mbalimbali za  binadamu mali ya Serikali. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe…(endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jana tarehe 21 Julai 2023, Kaimu Kamanda wa mkoa wa Songwe, Kamishna Msaidizi wa Polisi Rashid Ngonyani amesema mbinu aliyotumia ni kuficha katika mifuko ya salfeti Ili dawa hizo zisionekane kisha aende kuziuza maeneo ya Mlowo.

Kaimu Kamanda amebainisha  dawa hizo kuwa ni Ciprofloxacin box 10, belo 3 za vyandarua, Gauzen absorbent 2 PCs, Vidonge vya uzazi wa mpango Boxi 7, Gauze bunda 02 Surgical gloves boxi 10.

Kutokana na tukio hilo, Kamanda huyo ametoa wito wananchi kutojihusisha na uhalifu kwani Jeshi la Polisi halitosita kuchukua hatua kali dhidi yao.

Pia limewataka watumishi wa Serikali kuacha tamaa kwani Serikali imekuwa ikitumia fedha nyingi kwa ajili ya kununua vifaa mbalimbali pamoja na dawa kwa kwa ajili ya kuhudumia wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Hatuoni faida ya demokrasia

Spread the loveMwenyekiti wa Chadema, Fremaan Mbowe amesema Tanzania haijanufaika na miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ataka wananchi wasiruhusu bakora za Magufuli

Spread the loveMwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD), Profesa Ibrahimu Lipumba...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mbunge Mwakasaka alitaka Jeshi la Polisi kutenda haki

Spread the loveEMMANUEL Adamson Mwakasaka, Mbunge wa Tabora Mjini (CCM), amelitaka Jeshi...

Habari za SiasaTangulizi

Madeleka aibwaga Jamhuri kesi za kubambikiwa

Spread the loveWakili Peter Madeleka ameshinda rufaa yake namba 263 ya mwaka...

error: Content is protected !!