Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof Juma: Ukata umekwamisha utekelezaji mapendekezo Tume ya Jaji Bomani
Habari za Siasa

Prof Juma: Ukata umekwamisha utekelezaji mapendekezo Tume ya Jaji Bomani

Spread the love

JAJI Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahim Juma, amesema tume mbalimbali zimeundwa kwa ajili ya kukusanya maoni kuhusu maboresho ya haki jinai, lakini mapendekezo hayo yamekwama kutekelezwa kwa sababu ya ukosefu wa rasilimali fedha. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Prof. Juma ametoa kauli hiyo leo tarehe 15 Julai 2023, akizungumza katika hafla ya Rais Samia Suluhu Hassan, kupokea taarifa ya tume aliyounda kuangalia jinsi ya kuboresha haki jinai nchini, Ikulu jijini Dar es Salaam.

“Tume ya Jaji Bomani mapendekezo mengi hayakufanyika kwa sababu ya ukosefu wa fedha, zilitakiwa dola za marekani 285 milioni, kutekeleza mapendekezo yote lakini kutokana na ukosefu wa fedha yakawa yanateklezwa vipande vipande ndiyo maana unakuta sehemu kubwa hayakutekelezwa,” amesema Prof. Juma.

Kutokana na changamoto hiyo, Prof. Juma amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan, alitatue tatizo hilo kwa kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na tume hiyo inayoongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu, Othman Chande.

Naye Jaji Mkuu mstaafu wa Tanzania, Joseph Warioba, amesema mapendekezo hayo yakifanyiwa kazi itasaidia kuboresha utendaji wa taasisi za haki jinai nchini.
“Katika nchi yetu wakati wa amani sura ya dola ni vyombo vinavyoshughulika na haki jinai na mahakama na kazi waliyofanya itasaidia sana kwa wananchi kuelewa utaratibu wa haki jinai katika nchi yetu na pia itasaidia mahali ambapo tunahitaji kuimarisha ili vyombo hivi viweze kufanya kazi vizuri,” amesema Jaji Warioba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!