Saturday , 18 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mshahara wa milioni 28 kwa Rais Ruto wazua gumzo Kenya
KimataifaTangulizi

Mshahara wa milioni 28 kwa Rais Ruto wazua gumzo Kenya

Spread the love

RAIS wa Kenya, William Ruto, naibu wake Rigathi Gachagua na Katibu Mkuu Mkuu, Musalia Mudavadi kuwa ni moja ya maafisa wa ngazi ya juu serikali ya nchi hiyo wanaoongoza kwa mishahara mikubwa katika nyongeza ya mishahara iliyopendekezwa hivi karibuni. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Tume ya Mishahara ya nchi hiyo (SRC) ilichapisha mapendekezo hayo kwenye kalenda yake kwa mwaka wa kifedha 2023/2024.

Kwa mujibu wa pendekezo la mishahara, maafisa wa serikali watasubiriwa ongezeko la asilimia 14 kuanzia tarehe 1 Julai 2023.

Aidha, kutokana na taarifa hiyo, tayari mjadala umeanza kushika kasi katika mitandao ya kijamii hasa ikizingatiwa serikali hiyo imekuwa ikilia kuwa na ukata wa fedha.

Baada ya kuchukua hatamu za uongozi, Naibu rais Rigathi Gachagua alisema walihidi kupunguza makali ya maisha kwa wananchi kwa kupunguza baadhi ya gharama zisizo za lazima Serikali.

Bloga maarufu nchini humo Pauline Njoroge ni miongoni mwa wale ambao wameanza kuikosoa serikali akisema Kenya Kwanza wameharibu uchumi na sasa wanataka kula zaidi.

Ikiwa pendekezo litapitishwa, Rais atapokea KSh 1.65 milioni (TSh. 28.3 milioni) kuanzia Julai 1, 2024.

Naibu Rais atapata KSh 1,367,438 (Tsh. 23.4 milioni), kutoka KSh 1,227,188 (Tsh 21 milioni) na ongezeko lingine hadi KSh 1.4 milioni (Tsh. 24 milioni) Julai 1, 2024, ambayo ni ongezeko la 14%.

Katibu Mkuu Mkuu Musalia Mudavadi na mawaziri wengine watapokea KSh 1,056,000, kutoka KSh 924,000, kuanzia Julai 1, 2023.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Uingereza yamwaga bil. 9 kumuunga mkono Samia matumizi nishati

Spread the loveWaziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani...

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe abadili mbinu ya kudai Katiba mpya

Spread the loveMwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema), Fremaan Mbowe amebadili mbinu...

error: Content is protected !!