Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kata nne Musoma Vijijini mbioni kupata maji
Habari za Siasa

Kata nne Musoma Vijijini mbioni kupata maji

Spread the love

WANAVIJIJI kutoka kata nne za Wilaya ya Musoma Vijijini, mkoani Mara, wako mbioni kuondokana na adha ya huduma ya maji safi na salama baada ya miradi yake inayotarajiwa kukamilika hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa jana na Ofisi ya Mbunge wa Musoma Vijijini, Prof. Sospeter Muhongo, miradi ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza maji kutoka Ziwa Victoria, ipo mbioni kukamilika.

Taarifa hiyo imesema kuwa, mitambo ya kusukuma maji inayotengenezwa katika nchi za China, Hungary na Turkey, inatarajiwa kuwasilisha nchini kupitia mradi wa bomba kuu la maji la Mugango-Kiabakari-Butiama, unaogharimu Sh. 70.5 bilioni.

“Mradi huu uwezo wake wa kuzalisha maji ni Lita 35 milioni kwa siku. Katika Kata za Tegeruka na Mugango, Mbunge alienda kukagua ujenzi huo,” imesema taarifa hiyo.

Mbali na ujenzi wa mabomba ya kusambaza maji, pia ujenzi wa matenki ya maji unaendelea jimboni humo, ikiwemo tenki lenye ujazo wa Lita 135,000 linalojenhwa katika Kijiji Cha Kataryo.


“Wananchi wa Jimbo la Musoma Vijijini wanaishukuru Serikali yetu chini ya uongozi mzuri wa Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kutoa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji ya bomba vijijini mwetu,” imesema taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!