Saturday , 18 May 2024
Home Kitengo Biashara Mbarawa: Ufanisi bandarini hauridhishi
Biashara

Mbarawa: Ufanisi bandarini hauridhishi

Spread the love

WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa leo Jumamosi amewasilisha bungeni maelezo ya awali kuhusu mapendekezo ya kuridhia mkataba baina ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Dubai katika ushirikiano wa kiuchumi na kijamii kwa ajili ya uendelezaji na uboreshaji wa utendaji kazi wa bandari za Tanzania ambapo pamoja na mambo mengine amesisitiza kuwa hali ya sasa ya utendaji wa Bandari ya Dar es Salaam imeendelea kuwa ya kiwango cha chini ikilinganishwa na bandari shindani kikanda. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Amesema Serikali imeendelea kuwekeza kwenye bandari zake kwa vipindi tofauti kwa kutumia vyanzo vyake na fedha za mikopo katika kutekeleza mikakati kwa lengo la kuboresha sekta ya bandari nchini.

“Pamoja na kuchukua hatua mbalimbali za maboresho ya Bandari ya Dar es Salaam, bado ufanisi katika utoaji huduma za bandari haujafikia viwango vinavyotakiwa kimataifa.

“Kwa mfano, gharama ya kusafirisha kasha moja kutoka nje ya nchi (on transit) kwenda nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) zinafikia takriban Dola za Marekani kati ya 8,500 hadi 12,000. Hii ni gharama kubwa sana ikilinganishwa na Bandari shindani,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Cheza kasino sloti ya Fruit O Rama malipo unayapata kwa njia 10

Spread the love Karibu kwenye burudani ya kasino ya mtandaoni isiyozuilikayenye kutawaliwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua bima ya afya kwa wakulima

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na kampuni...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Total Energies yawekeza bilioni 17 kusambaza gesi ya kupikia

Spread the loveILI kurahisisha upatikanaji wa gesi ya kupikia kwa gharama nafuu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Taifa Gas waanika mikakati kupunguza gharama za gesi ya kupikia

Spread the loveKATIKA kuunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan kuhamasisha...

error: Content is protected !!