Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wassira: Mikataba mibovu inapoteza uaminifu wa wananchi kwa serikali
Habari Mchanganyiko

Wassira: Mikataba mibovu inapoteza uaminifu wa wananchi kwa serikali

Steven Wasira
Spread the love

 

MWENYEKITI wa Bodi ya Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), Stephen Wassira, amesema kitendo cha baadhi ya taasisi za Serikali kusaini mikataba mibovu bila kujali maslahi ya umma, kinapoteza uaminifu wa wananchi kwa viongozi wanaowaongoza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wassira ametoa kauli hiyo leo tarehe 20 Aprili 2023, jijini Dar es Salaam wakati akichangia mada katika mkutano wa Msajili wa Hazina na viongozi wa taasisi, mashirika na wenyeviti wa bodi za mashirika ya umma, uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Akitoa mfano kuhusu ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kwa 2021/22, amesema inatia aibu kuona mkataba wa mradi mkubwa kama wa ujenzi wa reli ya kisasa SGR unaitia hasara serikali.

“Sijui matatizo yetu yanatokana na nini? Kila siku kuna mikataba mibovu na hii inaharibu uaminifu wa wananchi wa Serikali,” amesema Wassira.

Mwanasiasa huyo mkongwe nchini, amehoji kama kitendo cha baadhi ya taasisi kama Shirika la reli Tanzania (TRC) kutoa zabuni kwa wakandarasi wenye gharama kubwa na kuacha wenye gharama ndogo, ni ukosefu wa elimu ya majadiliano au wizi.

“Tumesikia CAG anasema katika ujenzi wa reli wametoa tenda ambayo ingekuwa na thamani ya Sh. 600 bilioni, alikuwa mkandarasi mmoja wameingia akasema atatoa Sh. 1.7 trilioni halafu huyo akachukuliwa. Sasa huu ni ukosefu wa elimu ya kujadiliana au ni wizi? Unasema uende kwenye public utawaambia watanzania ulifanyaje mpaka ukatoka Sh. 600 bilioni mpaka Sh. 1.7 trilioni,” amesema Wassira.

Katika hatua nyingine, Wassira ameshauri tume ya mipango ya taifa iundwe ili kuwezesha viongozi wapya kuendeleza mambo yaliyoanza kufanywa na watangulizi wao.

“Kuwe na tume ya mipango ambayo itakuwa na kazi ya kupanga na uwekezaji, ambayo jambo jema kwa mawazo tungekuwe na vitu endelevu sio kila mtu anayekuja anachukua cha kwake, mwingine akija anafuta. Tunapata shida kidogo, amesema Wassira.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara yaomba bajeti ya Sh. 67.9 bilioni, wamachinga watengewa bilioni 10

Spread the loveBAJETI ya Wizara ya maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na...

Habari MchanganyikoTangulizi

Migogoro ya ndoa yaongezeka, Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveMIGOGORO ya ndoa na familia imeongezeka kwa asilimia 8.3  kutoka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yahamasisha uanzishaji vituo vya kulea watoto wachanga

Spread the loveSERIKALI imewahimiza wananchi kujenga vituo vya kulelea watoto wadogo na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

error: Content is protected !!