Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Ramadhan Omary achaguliwa kuwa Katibu wa Baraza la Wafanyakazi TMA
Habari Mchanganyiko

Ramadhan Omary achaguliwa kuwa Katibu wa Baraza la Wafanyakazi TMA

Spread the love

 

WAJUMBE wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) wamemchagua, Ramadhani Omary kuwa Katibu wa Baraza la Wafanyakazi wa TMA, kupitia kikao cha Baraza hili kinachoendelea Morogoro tarehe 03 na 04 Aprili 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Omary alichaguliwa kwa kupata kura 62 akifuatiwa na Katibu Msaidizi, Mecklina Merchades kura 32, jumla ya kura zilizopigwa ni 94. Uchaguzi huo umesimamiwa na Christina Matega, Afisa kazi kutoka Wizara ya Kazi na Ajira, Morogoro.

Katika hatua nyingine, Baraza hilo lilitambulisha wimbo wa TUGHE-Taifa na kuzindua rasmi kipeperushi maalumu na bango la TUGHE-TMA ambavyo vitatumika katika kuitangaza TUGHE-TMA kwenye majukwaa mbalimbali kupitia dhana ya uzalendo, ubunifu na uwajibakaji.

Omary ni Mchambuzi wa Hali ya Hewa kutoka Ofisi ya Kituo Kikuu cha Utabiri, dawati la utabiri wa muda mrefu, anachukua nafasi ya Chuki Sangalugembe aliyemaliza muda wake kwa mujibu wa mkataba wa Baraza la Wafanyakazi wa TMA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!