Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko TRC waendesha zoezi la kutwaa ardhi kwa ajili ya kupisha ujenzi wa SGR Tabora
Habari Mchanganyiko

TRC waendesha zoezi la kutwaa ardhi kwa ajili ya kupisha ujenzi wa SGR Tabora

Spread the love

SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) linaendelea na utekelezaji wa utwaaji ardhi kwa matumizi ya ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) mkoani Tabora katika kipande cha tatu Makutupora –Tabora. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TRC, timu ya maafisa wa TRC ilianza kwa kufanya uhamasishaji kwa viongozi wa Serikali kwa ngazi ya wilaya, vijiji na kata pamoja na wananchi ambao ni walengwa katika zoezi hilo.

Uhamasishaji umefanyika ukiwa na lengo la kuwaelimisha wananchi na viongozi kuhusu utaratibu na namna zoezi la kuhamisha makaburi litakavyoendeshwa kwa kuzingatia Sheria ya ardhi na kanuni za afya.

Mara baada ya uhamasishaji zoezi la kuhamisha makaburi lilianza rasmi katika kijiji cha Itulu, kata ya Ndevelwa Manispa ya Tabora ambapo jumla ya makaburi 74 yamehamishiwa katika  sehemu nyingine iliyotengwa na Serikali za vijiji kwa lengo la kupisha ujenzi wa reli ya kisasa.

Katika hatua nyingine, viongozi wa mkoa wametoa wito kwa Serikali ya kijiji na ndugu wa marehemu kutoa ushirikano wa kutosha ili kuhakikisha zoezi linaenda salama na hatimaye kukamilika na mkandarasi kuendelea na ujenzi wa reli ya kisasa ambao hadi sasa umefikia 5.52%

Sambamba na hivyo zoezi limesimamiwa na kuratibiwa na viongozi mbalimbali na wataalamu wa afya, wahandisi, maafisa ardhi, maafisa jamii, vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa vijiji, kata, tarafa na viongozi wa Dini.

Hata hivyo zoezi la uhamishaji makaburi ni endelevu kwa sasa limeanza kufanyika katika manispaa ya Tabora katika kijiji cha Itulu na badaye mkoani Singida katika wilaya ya Manyoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!