MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema Rais Samia Suluhu Hassan, amempandisha cheo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar ea Salaam (RPC), Jumanne Muliro kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizj wa Polisi (SACP). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumamosi na Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, SACP David Misime, uteuzi wa Kamanda Muliro, aliyekuwa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), amepandishwa cheo kuanzia tarehe 20 Februari 2022.
“Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Camillus M.Wambura anapenda kuwajulisha kuwa Dk. Samia Suluhu Hassan ,Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama,” imesema taarifa hiyo na kuongeza:
“Amempandisha cheo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Muliro Jumanne Muliro kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP).
Amepandishwa cheo hicho kuanzia tarehe 20 Februari 2023.”
Leave a comment