Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TRC waendesha zoezi la kutwaa ardhi kwa ajili ya kupisha ujenzi wa SGR Tabora
Habari Mchanganyiko

TRC waendesha zoezi la kutwaa ardhi kwa ajili ya kupisha ujenzi wa SGR Tabora

Spread the love

SHIRIKA la Reli Tanzania (TRC) linaendelea na utekelezaji wa utwaaji ardhi kwa matumizi ya ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) mkoani Tabora katika kipande cha tatu Makutupora –Tabora. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na TRC, timu ya maafisa wa TRC ilianza kwa kufanya uhamasishaji kwa viongozi wa Serikali kwa ngazi ya wilaya, vijiji na kata pamoja na wananchi ambao ni walengwa katika zoezi hilo.

Uhamasishaji umefanyika ukiwa na lengo la kuwaelimisha wananchi na viongozi kuhusu utaratibu na namna zoezi la kuhamisha makaburi litakavyoendeshwa kwa kuzingatia Sheria ya ardhi na kanuni za afya.

Mara baada ya uhamasishaji zoezi la kuhamisha makaburi lilianza rasmi katika kijiji cha Itulu, kata ya Ndevelwa Manispa ya Tabora ambapo jumla ya makaburi 74 yamehamishiwa katika  sehemu nyingine iliyotengwa na Serikali za vijiji kwa lengo la kupisha ujenzi wa reli ya kisasa.

Katika hatua nyingine, viongozi wa mkoa wametoa wito kwa Serikali ya kijiji na ndugu wa marehemu kutoa ushirikano wa kutosha ili kuhakikisha zoezi linaenda salama na hatimaye kukamilika na mkandarasi kuendelea na ujenzi wa reli ya kisasa ambao hadi sasa umefikia 5.52%

Sambamba na hivyo zoezi limesimamiwa na kuratibiwa na viongozi mbalimbali na wataalamu wa afya, wahandisi, maafisa ardhi, maafisa jamii, vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa vijiji, kata, tarafa na viongozi wa Dini.

Hata hivyo zoezi la uhamishaji makaburi ni endelevu kwa sasa limeanza kufanyika katika manispaa ya Tabora katika kijiji cha Itulu na badaye mkoani Singida katika wilaya ya Manyoni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!