Saturday , 18 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto amkumbuka Maalim Seif
Habari za SiasaTangulizi

Zitto amkumbuka Maalim Seif

Spread the love

 

KIONGOZI wa Chama Cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amesema chama chake kinaendelea kumuenzi aliyekuwa Mwenyekiti wake Taifa, Maalim Seif Shariff Hamad, aliyefariki Dunia tarehe 17 Februari 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akitoa ujumbe wake wa kumbukumbu ya miaka miwili ya kifo Cha Maalim Seif, leo tarehe 17 February 2023, kupitia ukurasa wake wa Twitter, Zitto amesema ACT-Wazalendo itaendeleza harakati zake kuimarisha demokrasia na kupigania muungano wa haki nchini.

“Tunakuenzi kwa kuendeleza harakati za kuimarisha demokrasia nchini na kupigania muungano wa haki, heshima na usawa. Tunaendelea kusimamia maridhiano ya Wazanzibari na kuongoza juhudi za maridhiano ya Watanzania. Tunakukumbuka kwa vitendo Maalim!,” ameandika Zitto.

Maalim Seif pamoja na wafuasi wake, walijiunga na ACT-Wazalendo 2019, kupitia opereshenj yake ya shusha tanga, pandisha tanga, wakitokea Chama cha Wananchi (CUF), baada ya kukosa muafaka katika mgogoro wa kiuongozi uliokuwa unakikabili chama hicho, baada ya Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, kumtambua Prof. Ibrahim Lipumba, kuwa mwenyekiti halali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Uingereza yamwaga bil. 9 kumuunga mkono Samia matumizi nishati

Spread the loveWaziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani...

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe abadili mbinu ya kudai Katiba mpya

Spread the loveMwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema), Fremaan Mbowe amebadili mbinu...

error: Content is protected !!