Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa AAFP wapuliza kipyenga mikutano ya hadhara
Habari za Siasa

AAFP wapuliza kipyenga mikutano ya hadhara

Spread the love

CHAMA cha Wakulima nchini (AAFP), kimetangaza mpango wa kuanza kufanya mikutano ya hadhara kuanzia Februari 2023, baada ya kufanya mkutano wake mkuu kesho Jumapili, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumamosi, tarehe 11 Februari 2023 na Mwenyekiti wa AAFP Taifa, Said Sudi Said, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, kwenye Uchaguzi wa Jukwaa la Wanawake na Vijana la chama hicho.

“Mikutano ya hadhara ni haki yetu, chama kinategemea kuanza mikutano lakini katika mazingira ya uadilifu sababu sio sehemu ya kufanya fujo, bali ni sehemu ya kufanya maendeleo na kueleza ushauri wetu juu ya namna gani ya kupata yale tunayohitaji. Katika demokrasia huwezi sema kiongozi hafai sababu unayotaka hayatekelezwi unapaswa kuyaeleza ili yatekelezwe,” amesema Said.

Said amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuruhusu mikutano ya hadhara, huku akiusifu uongozi kwamba umekuwa chachu Kwa wanawake nchini katika kufikia nafasi za juu za uongozi wa nchi.

Akizungumzia uchaguzi huo, Said amewataka wajumbe kuchagua viongozi imara watakaonisaidia chama hicho kupata matokeo mazuri katika chaguzi zijazo.

Naye Kaimu Makamu Mwenyekiti wa AAFP Taifa, Nancy Mrikaria, amewataka viongozi wa jukwaa la wanawake watakaochaguliwa wahakikishe wanakiinarisha chama ili kipate wanachama wengi zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!