Saturday , 18 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hoja ya Moshi kuwa Jiji yaibuliwa tena bungeni
Habari za Siasa

Hoja ya Moshi kuwa Jiji yaibuliwa tena bungeni

Spread the love

 

MBUNGE wa Moshi Mjini, Priscus Tarimo, ameitaka Serikali kupandisha hadhi ya utawala miji iliyokidhi vigezo, pamoja na kugawa mikoa yenye ukubwa wa kijiografia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo kwa Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, leo Alhamisi, bungeni jijini Dodoma, Tarimo ameihoji Serikali kwa nini isipandishe hadhi halmashauri zilizokidhi vigezo vya kuwa jiji ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Moshi.

“Nini mpango wa Serikali kugawa au kuongeza na kupandisha hadhi maeneo ya kiutawala ambayo yamekidhi vigezo? Kugawa, kuongeza au kupandisha hadhi maeneo ya kiutawala ambayo yamekidhi vigezo? Mfano kugawa mikoa mikubwa kama Tanga na Morogoro au kupandisha hadhi halmashauri kuwa majiji kama Halmashauri ya Manispaa Moshi?” amehoji Tarimo.

Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, alimtaka Waziri Majaliwa asilijibu swali hilo akisema ni mahususi kujibiwa na mawaziri wa kisekta.

“Hili manispaa ya Moshi nadhani yenyewe liko mahususi linahitaji lijibiwe na mawaziri wa kisekta,” amesema Spika Tulia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Uingereza yamwaga bil. 9 kumuunga mkono Samia matumizi nishati

Spread the loveWaziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani...

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe abadili mbinu ya kudai Katiba mpya

Spread the loveMwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema), Fremaan Mbowe amebadili mbinu...

error: Content is protected !!