Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanawake wachimbaji wajenga zahanati kuokoa afya za wakazi 2000
Habari Mchanganyiko

Wanawake wachimbaji wajenga zahanati kuokoa afya za wakazi 2000

Spread the love

 

ZAIDI wakazi 2,000 wa kijiji cha Nyamishiga Kata ya Lunguya Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga wameondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kilomita 15 kufuata huduma za Afya Lunguya baada ya mgodi uliopo katika eneo hilo kujenga Zahanati kijijini hapo. Anaripoti Paul Kayanda, Kahama … (endelea).

Hatua ya ujenzi wa kituo cha afya ni juhudi za kikundi cha wanawake wanaojishughulisha na shughuli za uchimbaji wa dhahabu katika Halmashauri ya Msalala ambacho kilipewa dhamana na serikali ya kusimamia maduhuli na tozo mbalimbali kwenye eneo lenye mfumuko wa madini ya dhahabu ‘rush’ katika kijiji hicho.

Wakizungumzia ujenzi wa zahanati hiyo ambayo imekamilika kwa asilimia 80 baadhi ya wanawake hao Semeni John ambaye pia ni mwenyekiti wa mgodi huo wamesema wanajivunia kujenga Zahanati kupitia fedha za wajibu wa kampuni kwa jamii (CSR).

Amesema fedha hizo kiasi cha Sh milioni 200 waliyokusanya imewezesha zahanati hiyo kujengwa hadi kufikia asilimia 80 ya ujenzi.

Naye Katibu wa mgodi huo, Hilda Jackson amesema wataendelea kuhamasisha wanawake kuingiza kwenye shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu badala ya kuwaachia wanaume peke yao.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Kijiji cha Nyamishiga, Diwani wa Kata ya Lunguya, Benedicto Manwari amesema wananchi wamefurahishwa na kitendo cha mgodi kuangalia eneo muhimu la huduma ya wananchi wote.

“Changamoto ya wananchi kuhangaika kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta matibabu inaondoka, mpaka sasa wananchi wanapata huduma kwa tabu kwani wanalazimika kutembea umbali mrefu wa kilomita 15 kwenda Lunguya Katani.

“Nyakati za usiku ni shida, wajawazito wanaofikia muda wa kujifungua ikitokea amepatwa na uchungu usiku ni shida,” amesema Diwani huyo.

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala, Flora Sagasaga amesema uwepo wa zahanati hiyo itasaidia pia wachimbaji wadogo wanaofanya shughuli zao kwenye mgodi huo pindi wanapopata majeraha madogomadogo.

Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Wadogo mkoa wa Shinyanga, Hamza Tandiko ameiomba serikali kupitia tume ya madini iwarasimishe akinamama hao na kuwapatia leseni ya uchimbaji ili wakusanye vyema maduhuli ya serikali pamoja na kuendelea kunufaisha wakazi wa Kijiji na maeneo mengine.

Naye Afisa Madini Mkazi mkoa wa Kimadini Kahama, Mhandisi Jeremia Hango akijibu ombi la leseni kwa akina mama hao amesema atalifikisha kwa wahusika wa kitengo cha leseni makao makuu jijijini Dodoma.

Amesema wanawake hao iwapo watapata leseni watachimba kwa bidii na tija zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

error: Content is protected !!