Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanawake wachimbaji wajenga zahanati kuokoa afya za wakazi 2000
Habari Mchanganyiko

Wanawake wachimbaji wajenga zahanati kuokoa afya za wakazi 2000

Spread the love

 

ZAIDI wakazi 2,000 wa kijiji cha Nyamishiga Kata ya Lunguya Halmashauri ya Msalala wilayani Kahama mkoani Shinyanga wameondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kilomita 15 kufuata huduma za Afya Lunguya baada ya mgodi uliopo katika eneo hilo kujenga Zahanati kijijini hapo. Anaripoti Paul Kayanda, Kahama … (endelea).

Hatua ya ujenzi wa kituo cha afya ni juhudi za kikundi cha wanawake wanaojishughulisha na shughuli za uchimbaji wa dhahabu katika Halmashauri ya Msalala ambacho kilipewa dhamana na serikali ya kusimamia maduhuli na tozo mbalimbali kwenye eneo lenye mfumuko wa madini ya dhahabu ‘rush’ katika kijiji hicho.

Wakizungumzia ujenzi wa zahanati hiyo ambayo imekamilika kwa asilimia 80 baadhi ya wanawake hao Semeni John ambaye pia ni mwenyekiti wa mgodi huo wamesema wanajivunia kujenga Zahanati kupitia fedha za wajibu wa kampuni kwa jamii (CSR).

Amesema fedha hizo kiasi cha Sh milioni 200 waliyokusanya imewezesha zahanati hiyo kujengwa hadi kufikia asilimia 80 ya ujenzi.

Naye Katibu wa mgodi huo, Hilda Jackson amesema wataendelea kuhamasisha wanawake kuingiza kwenye shughuli za uchimbaji wa madini ya dhahabu badala ya kuwaachia wanaume peke yao.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Kijiji cha Nyamishiga, Diwani wa Kata ya Lunguya, Benedicto Manwari amesema wananchi wamefurahishwa na kitendo cha mgodi kuangalia eneo muhimu la huduma ya wananchi wote.

“Changamoto ya wananchi kuhangaika kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta matibabu inaondoka, mpaka sasa wananchi wanapata huduma kwa tabu kwani wanalazimika kutembea umbali mrefu wa kilomita 15 kwenda Lunguya Katani.

“Nyakati za usiku ni shida, wajawazito wanaofikia muda wa kujifungua ikitokea amepatwa na uchungu usiku ni shida,” amesema Diwani huyo.

Kwa upande wake Makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya Msalala, Flora Sagasaga amesema uwepo wa zahanati hiyo itasaidia pia wachimbaji wadogo wanaofanya shughuli zao kwenye mgodi huo pindi wanapopata majeraha madogomadogo.

Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimbaji Wadogo mkoa wa Shinyanga, Hamza Tandiko ameiomba serikali kupitia tume ya madini iwarasimishe akinamama hao na kuwapatia leseni ya uchimbaji ili wakusanye vyema maduhuli ya serikali pamoja na kuendelea kunufaisha wakazi wa Kijiji na maeneo mengine.

Naye Afisa Madini Mkazi mkoa wa Kimadini Kahama, Mhandisi Jeremia Hango akijibu ombi la leseni kwa akina mama hao amesema atalifikisha kwa wahusika wa kitengo cha leseni makao makuu jijijini Dodoma.

Amesema wanawake hao iwapo watapata leseni watachimba kwa bidii na tija zaidi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!