Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Uchaguzi wenyeviti wa CCM wilaya kuanza Oktoba mosi
Habari za Siasa

Uchaguzi wenyeviti wa CCM wilaya kuanza Oktoba mosi

Katibu wa Itikadi na uenezi CCM, Shaka Hamidu Shaka
Spread the love


KATIBU wa itikadi na uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),  Shaka Hamdu Shaka amewasisitiza wanachama wa chama hicho kujitokeza kwenye uchaguzi wa ngazi ya Wilaya tarehe 1 na 2 Octoba, 2022.  Anaripoti Helena Mkonyi. TUDARCo … (endelea).

Uteuzi huo wa mwisho wa  wagombea uwenyekiti  wa wilaya  katika Wilaya 168 nchini,  umefanyika leo Jijini Dodoma chini ya Mwenyekiti wa CCM Rais Samia Suluhu Hassan.

Shaka amesema “Tumeteuwa na tumeshapata wagombea ambao wataenda kusimama kwenye uchaguzi wa ngazi ya Wilaya tarehe 1 na 2 Ockoba 2022”.

Shaka amewaomba wanachama wajitokeze kwa wingi  katika uchaguzi wa wenyeviti wa CCM ngazi ya Wilaya ambao hufanyika kila baada ya miaka mitano kwa mujibu wa katiba yao.

Aidha amesema kwamba Halmashauri kuu ya Taifa imeongeza muda wa kuchukua fomu na kurejesha fomu kwa ngazi ya Taifa na Mkoa kwa upande wa Zanzibar na Tanzania bara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!