Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko ‘Viongozi wasitumia miradi kuhalalisha tozo’
Habari Mchanganyiko

‘Viongozi wasitumia miradi kuhalalisha tozo’

Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maaskofu na Mashehe ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Madhehebu ya Dini nchini Askofu William Mwamalanga
Spread the love

VIONGOZI wa dini wamewataka viongozi wa serikali kuacha kutumia kigezo cha ujenzi wa  miradi ya afya, elimu, maji na mingine, ili kuhalalasha tozo ambayo imeibua malalamiko kila kona ya nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endele).

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 5 Septemba, 2022 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Maaskofu na Mashehe ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Madhehebu ya Dini nchini Askofu William Mwamalanga alisema viongozi hao hawakubaliana mfumo huo kwa kuwa unaumiza wananchi.

Askofu Mwamalanga alisema walikuwa na kongamano lililoshirikisha viongozi wa dini na kutoka na kauli ya moja ya kupinga tozo kwa kuwa inaonekana ni kuwalipisha wananchi kodi mara mbili.

Alisema kinachosemwa na viongozi hao na kinachoonekana mitaani ni vitu tofauti hivyo kuwataka viongozi hao kufikiria njia nyingine ya kupata fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi.

“Baadhi ya mawaziri wamekuwa wakitumia hoja ya utekelezaji wa miradi kama sababu ya kuwepo kwa tozo, ila ukipia huko mitaani hali ni tofauti miradi haitekelezwe, lakini kubwa zaidi ni ugumu wa maisha kwa sasa,” alisema.

Askofu Mwamalanga alisema tozo haziwezi kujenga nchi  kwani tafsiri ya tozo ni sawa na kumnyang’anyi watu ambao hawana sifa ya kutozwa tozo hizo.

“Unapoweka tozo maana yake huchagui mchangiaji awe mlemavu wa kuona, kusikia, viungo au maskini yoyote lazima alipe kama anatumia simu, hii sio sawa,” alisema.

Alisema wanachokiona kwa sasa ni kujenga taifa la waongo wanaongoza wananchi kwa ndimi za udanyifu na kutengeneza uchumi wa kiini macho  kila uchao.

Mwamalanga  amemuomba Rais    Samia Suluhu Hassan, kutumia wataalam wa uchumi kutoka Zambia  ili waje wasaidie kufufua uchumi  wa madini, mifugo, uvuvi na sekta nyingine ambazo hazitumiki ipasavyo, ili kuachana na tozo.

Alisema kutokana na Zambia kuwa na mipango mizuri  wafanyabiashara wakitanzania wanaenda kuwekeza katoka nchi hiyo, hali ambayo imesababisha fedha yao kuwa na thamani kuliko ya Tanzania kwa muda mfupi wa uongozi wa Rais Hakainde Hichilema.

Askofu Mwamalanga alisema Tanzania inapitia changamoto za kiuchumi kutokana na aina ya viongozi ambao wamepewa fursa ya kuongoza sekta nyeti kukosa uadilifu na ubunifu.

“Huwezi kujenga nchi kwa kunyanganya watu wako fedha mifukoni. Kusema kweli hawa wasaidizi wa Rais Samia wanaofikiria tozo hawawezi kukuza uchumi, ni vema wapumzike, ili waweze kumpa nafasi Rais Samia kufanya uteuzi mwingine,” alisema.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!