Saturday , 18 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo: Madeni ya Serikali yameifilisi NHIF
Habari za Siasa

ACT-Wazalendo: Madeni ya Serikali yameifilisi NHIF

Spread the love

MSEMAJI wa sekta ya uwekezaji, mashirika ya umma na hifadhi ya jamii wa ACT wazalendo, Mwanaisha Mndeme, amesema kuanzia mwaka 2018 hadi 2022 Shirika la Taifa la Bima ya Afya (NHIF) limejiendesha kwa hasara kutokana na madeni yaliyokopwa na Serikali. Anaripoti Apaikunda Mosha TUDARCo … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano ya tarehe 31, Agosti 2022, katika ofisi ya chama hicho amesema mfuko wa bima umekuwa ukileta vifurushi vipya, kuwatoza wananchi gharama zaidi na kupunguza mafao wanayopata wananchi ili kufidia makosa yake na mkusisitiza kuwa wananchi hawapaswi kulipa gharama kwa maamuzi mabovu ya Serikali.

Mndeme amesema kufuatia ripoti ya mkaguzi na mthibiti wa hesabu za serikali (CAG) mfuko huo umepata hasara ya Sh. 1.5 billion kutokana na ukusanya hafifu wa madeni, utoaji wa mikopo na uwekezaji mbovu wa fedha za umma.

Aidha, ameitaka serikali kupitia wizara ya fedha ihakikishe mikopo yote inayodaiwa kupitia mashirika ya umma na wizara kurudishwa haraka ili kuupa uwezo mfuko wa taifa wa bima ya afya kujiendesha wenyewe na kusaidia kila mtanzania kupata huduma bora ya afya.

Aidha, ameeleza kuwa 85% ya nguvu ya watanzania hawapo katika mfumo wa bima ya afya na ameitaka serikali kuhakikisha mifuko ya hifadhi ya jamii inaunganishwa na huduma ya afya ili kuhakikisha kuwa kila mtanzania anaweza kupata huduma ya afya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!