Saturday , 18 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mdee, wenzake wafika mahakamani, kesi yaanza kunguruma
Habari za SiasaTangulizi

Mdee, wenzake wafika mahakamani, kesi yaanza kunguruma

Spread the love

 

KWA mara ya kwanza Halima Mdee na wenzake sita, ambao ni Wabunge wa Viti Maalum waliofukuzwa uanachama wa Chadema, wamefika mahakamani kuitika wito wa mahakama. Anaripoti Faki Sosi na Apaikunda Mosha, Dar es Salaam … (endelea).

Awali tarehe 29 Julai mwaka huu Mahakama hiyo ilikubali ombi la Mawakili wa Chadema lililowasilishwa na Peter Kibatala la kutaka waombaji saba kwenye kesi ya kupinga kuvuliwa uanachama wa Chadema, kufika mahakamani hapo.

Mdee na wenzake wameomba mahakama hiyo kutengua kuvuliwa kwa uanachama wao ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Shauri hilo limeanza kusikilizwa saa tano kamili ambapo Jaji Cyprian Mkeha ameanza kusikiliza pingamizi la upande wa waombaji .

Pingamizi hilo limewasilishwa kupinga kiapo kinzani cha upande wa wajibu maombi namba moja (Chadema).

Endelea kusoma MwanaHALISI Online kujua zaidi kinachoendelea mahakamani hapo

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!