Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Mwamalanga amtaka IGP Wambura kuwatimua askari wanaokiuka haki za raia
Habari Mchanganyiko

Askofu Mwamalanga amtaka IGP Wambura kuwatimua askari wanaokiuka haki za raia

Spread the love

MWENYEKITI wa Kamati ya Kitaifa ya  Maaskofu na Mashehe ya Maadili, Amani na Haki za Binadamu  kwa jamii ya Madhehebu  nchini Askofu William Mwamalanga amempongeza Mkuu Mpya wa Jeshi la Polisi (IGP), Camilius Wambura huku akimtaka awafute kazi askari wanaokiuka haki za raia. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Askofu Mwamalanga ameyasema hayo kwenye taarifa aliyotoa kwa vyombo vya habari siku chache baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kumteua kuwa IGP akichukua nafasi ya IGP Simon Sirro ambaye ameteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zimbambwe.

“Sisi viongozi wa dini  tunamshauri IGP Wambura kulijenga jeshi  litakalo kumbatia raia mwema  badala ya kuyakumbatia magenge ya rushwa, vigogo wa dawa za kulevya, majambazi, waongo na vigogo wa Serikali wanaofisadi mali za umma  raia wema ndiyo silaha muhimu kwa polisi kutokomeza wahalifu kuliko ilivyo sasa hivi,” alisema.

Askofu Mwamalinga  alisema duniani kote mataifa yanayofanikiwa , mchango mkubwa unachangiwa na  jeshi la polisi, hivyo imani yao ni kuona chombo hicho kinachochea maendeleo  ya jamii.

Alisema iwapo jeshi hilo litakumbatia  raia wema  na taifa litakuwa na jamii yenye  uadilifu na kupenda amani kuliko kuwa na polisi wanaowafundisha  wahalifu  mbinu za uhalifu.

Aidha  Askofu Mwamalanga amemkumbusha IGP Wambura kuwa amani ni msingi wa haki  na kumuomba  atembelee vituo vyote vya polisi nchini ili ajionea  uvunjifu mkubwa wa haki za raia wema wakiwamo askari polisi wa vyeo vya chini ambao huwekwa lokapu  na wakubwa zao bila sababu za msingi.

Mwamalanga alimuomba IGP Wambura kuhakikisha anatengeneza jeshi ambalo litafuata misingi ya jeshi hilo na sio kujihusisha na siasa hali ambayo inashusha heshima ya jeshi hilo.

“Tunataka kuona jeshi ambalo litafuata PGO katika kutekeleza majukumu yake na sio maagizo ya viongozi wa kisiasa, kwani asilimia kubwa yanaumiza wananchi,” alisema.

1 Comment

  • Ni Vizuri Raia, Wajenge Urafiki na Askali Wanaowalinda! Ukimuona Police Uone Amani Furaha, Uamini Huko Salama! Sio Kumuona Police, Ukaona ni Adui Mkubwa Kuliko Huyo Mkosaji! Asante Saana Bishop Mwamaranga! Nafikili Hii Itafika Mahali Husika!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!