Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watatu mbaroni tuhuma kumjeruhi mtendaji Kata Morogoro
Habari Mchanganyiko

Watatu mbaroni tuhuma kumjeruhi mtendaji Kata Morogoro

Pingu
Spread the love

 

JESHI la Polisi Mkoa wa Morogogo nchini Tanzania linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kumshambulia Geoge Kaloya, ofisa mtendaji wa Kijiji ya Chilombira wilayani Mahenge kwa kitu chenye ncha kali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogogo, Fortunatus Musilim akizungumza na MwanaHALISI Online amesema watuhumiwa hao walimshambuliwa Kaloya tarehe 17 Juni 2022 katika eneo la Katope alipokwenda kutekeleza majukumu yake ya kazi akikaimu nyadhifa ya Mtendaji wa Tarafa ya Ruaha.

Kamanda Musilim amesema ofisa huyo alikuwa akiwaondoa wachimbaji madini wasiokuwa na vibali kwenye eneo la Kitope ndio watuhumiwa hao wakamshambuliwa.

Amewataja wanaoshikiliwa Twaiba Masikini (56) mkazi wa Kijiji cha Togo, Osward Sixbelt (36) na William Ali (65) kwa tuhuma za kumjeruhi Ofisa huyo.

Ofisa huyo amelazwa Hospitali ya St. Fransics ya Ifakara akiendelea na matababu.

“Upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani watuhumiwa hao,” amesema Kamanda Musilim.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Dodoma akabidhiwa bunduki mbili za wahalifu

Spread the love  Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa ya Kulevya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yazindua huduma maalum kwa wastaafu

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua huduma maalum kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yazindua akaunti ya Kikundi

Spread the loveBenki ya NMB imezindua akaunti ya kikundi yenye  maboresho makubwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi waidai STAMICO mishahara ya bilioni 1

Spread the loveWALIOKUWA wafanyakazi wa mgodi wa Shirika la Madini la Taifa...

error: Content is protected !!