Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Watatu mbaroni tuhuma kumjeruhi mtendaji Kata Morogoro
Habari Mchanganyiko

Watatu mbaroni tuhuma kumjeruhi mtendaji Kata Morogoro

Pingu
Spread the love

 

JESHI la Polisi Mkoa wa Morogogo nchini Tanzania linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kumshambulia Geoge Kaloya, ofisa mtendaji wa Kijiji ya Chilombira wilayani Mahenge kwa kitu chenye ncha kali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Morogoro … (endelea).

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogogo, Fortunatus Musilim akizungumza na MwanaHALISI Online amesema watuhumiwa hao walimshambuliwa Kaloya tarehe 17 Juni 2022 katika eneo la Katope alipokwenda kutekeleza majukumu yake ya kazi akikaimu nyadhifa ya Mtendaji wa Tarafa ya Ruaha.

Kamanda Musilim amesema ofisa huyo alikuwa akiwaondoa wachimbaji madini wasiokuwa na vibali kwenye eneo la Kitope ndio watuhumiwa hao wakamshambuliwa.

Amewataja wanaoshikiliwa Twaiba Masikini (56) mkazi wa Kijiji cha Togo, Osward Sixbelt (36) na William Ali (65) kwa tuhuma za kumjeruhi Ofisa huyo.

Ofisa huyo amelazwa Hospitali ya St. Fransics ya Ifakara akiendelea na matababu.

“Upelelezi ukikamilika tutawafikisha mahakamani watuhumiwa hao,” amesema Kamanda Musilim.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!