Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NCCR-Mageuzi yatangaza sekretarieti mpya, baada ya kuing’oa ile ya Mbatia
Habari za Siasa

NCCR-Mageuzi yatangaza sekretarieti mpya, baada ya kuing’oa ile ya Mbatia

Joseph Selasini, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya NCCR Mageuzi
Spread the love

 

CHAMA cha NCCR-Mageuzi, kimetangaza baadhi ya wajumbe wapya wa Sekretarieti ya chama hicho, baada ya kuvunja iliyokuwa inaongozwa na Mwenyekiti wake, James Mbatia, anayedaiwa kusimamishwa uongozi na Halmashauri Kuu yake, Mei 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wajumbe hao wametangazwa leo Ijumaa, tarehe 17 Juni 2022 na Katibu Mkuu wa NCCR-Mageuzi, Martha Chiomba, katika ofisi za makao makuu ya chama hicho, Ilala jijini Dar es Salaam.

Miongoni mwa wajumbe hao ni Joseph Selasini, aliyeteuliwa kuwa Katibu wa Idara ya Uenezi. Joseph Magabe (Idara ya Fedha, Uchumi na Mipango), Hassan Said (Idara ya Katiba, Sheria, Haki za Binadamu).

“Selasini atakuwa mwenezi wetu na kijiti kikubwa tunamuachia yeye azunguke kwa sapoti yangu. Tutazunguka naye nchi nzima na sasa tunamaanisha hakitakuwa chama cha mikutano ya wanahabari, hiki ni chama cha wananchi, tutarudi kwa wananchi kwa vitendo,” amesema Chiomba.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Haji Khamis, amesema mkutano mkuu wa chama hicho utaitishwa wakati wowote kuanzia sasa, huku akidai hawana migogoro kwa kuwa imeshatatuliwa na Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho iliyoketi Dar es Salaam, Mei 21, 2022 na kumsimamisha uongozi aliyekuwa Mbatia na sekretarieti yake.

“Masuala ya vikundi, majungu, mitafaruku iwe basi. Kuanzia sasa chama kimerudi kikiwa kimoja na mkutano mkuu wa taifa utakaoitishwa wakati wowote kutoka sasa utaleta maamuzi ya muafaka ambayo huwa yatategemea kutoka maamuzi ya halmashauri kuu ya taifa,” amesema Khamis.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!