Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Vigogo jiji la Arusha kizimbani kwa uhujumu uchumi
Habari Mchanganyiko

Vigogo jiji la Arusha kizimbani kwa uhujumu uchumi

Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imewapandisha kizimbani aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Dk. John Pima na wenzake wanne kwa mashitaka kutenda makosa nane katika kesi za uhujumu uchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Washitakiwa hao wamepandishwa kizimbani leo Ijumaa tarehe 17, Juni, 2022 katika mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha.

Pamoja na Dk. Pima washitakiwa wengine walipandishwa kizimbani ni waliokuwa wachumi wa jiji, Innocent Maduhu, Nuru Ginana na Alex Daniel na Mwwekahazina wa Jiji, Mariam Mshana ambaye hakuwepo mahakamani hapo.

Hata hivyo upande wa Jamhuri umeiomba Mahakama kutoa hai ya wito na kukamatwa kwa mshatakiwa huyo ambaye ni wapili katika kesi zote.

Wakisomewa mashitaka mbele ya Hakimu Mkazi Bittony Mwakizu, katika kesi ya kwanza Dk. Pima, Mariam, Maduhu na Ginana wanakabiliwa na mashitaka manne ikiwemo ufujaji na ubadhirifu, matumizi ya nyaraka kwa lengo la kumdanganya mwajiri.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai Mosi, 2022 ambapo washitakiwa watasomewa maelezo ya awali.
Itakumbukwa Mei 24 mwaka huu Waziri Mkuu KAssim Majaliwa aliwasimamisha kazi vigogo hao kwa tuhuma za ubadhirifu na kuagiza uchunguzi ufanyike na endapo watabainika kutenda makosa hao wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!