Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa aagiza Uhamiaji kuzuia Paspoti za wakandarasi MV Mwanza
Habari MchanganyikoTangulizi

Majaliwa aagiza Uhamiaji kuzuia Paspoti za wakandarasi MV Mwanza

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akikagua Ujenzi wa Meli mpya ya Mv.Mwanza Hapa Kazi tu katika Bandari ya Mwanza Kusini.
Spread the love

WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameagiza Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mwanza kuzishikilia paspoti za wafanyakazi wa Kampuni ya Gas Entec Ship-building Engineering ya nchini Korea ambayo inayojenga Meli mpya ya Mv. Mwanza Hapa Kazi tu katika Bandari ya Mwanza Kusinikwa kukiuka madharti ya mkataba wa kazi hiyo.

Ujenzi wa meli hiyo mpya inagharimu zaidi ya Sh billioni 97 ambapo mpaka sasa Serikali imelipa zaidi ya asilimia 80 ya fedha zote ilihali ujenzi wake umefikia asilimia 65 pekee. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mkandarasi wa mradi huu amefukuza wafanyakazi zaidi ya 100 na kubaki na wafanyakazi 20 tu

Majaliwa ametoa maagizo hayo leo tarehe 7 Mei, 2022 katika ziara yake ya siku nne ambayo ameanza kuifanya leo mkoani humo.

Amesema lengo la kuchukua uamuzi unatokana na Kampuni hiyo kuondoa wafanyakazi zaidi ya 100 waliokuwa wanajenga Meli hiyo na kubakiza wafanyakazi 20.

Amesema kwa mujibu wa mkataba ujenzi wa meli hiyo hadi kufikia leo Mei 7, 2022 ulitakiwa uwe umefikia asilimia 95.

Pia kampuni hiyo imeuza hisa kwa Kampuni nyingine bila Serikali kujua jambo ambalo ni kinyume na mkataba wa Kampuni hiyo na Serikali ya Tanzania.

“Nawaagiza Uhamiaji ichukue Passpoti zote za wakandarasi hadi meli ikamilike, nimezungumza na Balozi wa Korea ameridhia, nimewasiliana na Rais naye ameridhia,” amesema Majaliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

error: Content is protected !!