WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameagiza Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Mwanza kuzishikilia paspoti za wafanyakazi wa Kampuni ya Gas Entec Ship-building Engineering ya nchini Korea ambayo inayojenga Meli mpya ya Mv. Mwanza Hapa Kazi tu katika Bandari ya Mwanza Kusinikwa kukiuka madharti ya mkataba wa kazi hiyo.
Ujenzi wa meli hiyo mpya inagharimu zaidi ya Sh billioni 97 ambapo mpaka sasa Serikali imelipa zaidi ya asilimia 80 ya fedha zote ilihali ujenzi wake umefikia asilimia 65 pekee. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Majaliwa ametoa maagizo hayo leo tarehe 7 Mei, 2022 katika ziara yake ya siku nne ambayo ameanza kuifanya leo mkoani humo.
Amesema lengo la kuchukua uamuzi unatokana na Kampuni hiyo kuondoa wafanyakazi zaidi ya 100 waliokuwa wanajenga Meli hiyo na kubakiza wafanyakazi 20.
Amesema kwa mujibu wa mkataba ujenzi wa meli hiyo hadi kufikia leo Mei 7, 2022 ulitakiwa uwe umefikia asilimia 95.
Pia kampuni hiyo imeuza hisa kwa Kampuni nyingine bila Serikali kujua jambo ambalo ni kinyume na mkataba wa Kampuni hiyo na Serikali ya Tanzania.
“Nawaagiza Uhamiaji ichukue Passpoti zote za wakandarasi hadi meli ikamilike, nimezungumza na Balozi wa Korea ameridhia, nimewasiliana na Rais naye ameridhia,” amesema Majaliwa.
Leave a comment