Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Samia: Kamilisheni Sheria kulinda taarifa binafsi za watu
Habari za Siasa

Samia: Kamilisheni Sheria kulinda taarifa binafsi za watu

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan ameielekeza Wizara ya Habari na Teknolojia ya Mawasiliano ya Habari kuhakikisha inakamilsha Sheria ya kulinda taarifa binafsi za watu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Ametoa maelekezo hayo leo Jumatano tarehe 6 Aprili 2022, akizindua mfumo wa usafirishaji wa dharura wa wajawazito na watoto wachanga (M-Mama) jijini Dodoma.

Mkuu huyo wa nchi amesema sheria hiyo itasaidia pia kulinda taarifa za wajawazito zitakazokuwa zinatolewa kwenye mfumo wa M-Mama zisitumike tofauti na ilivyokusudiwa.

“Sio taarifa zimeshakusanywa mama huyo kachukuliwa taarifa zake tumbo lina sentomita ngapi motto yukoje tumboni, taarifa tunazikuta mitandaoni zinasambaa. Hapana.

“Ile Sheria ya kulinda taarifa za watu naomba ikamilishwe na taarifa hizo ziende zikalindwe,” amesema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!