Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bei petroli yafika 3,105 kwa lita
Habari Mchanganyiko

Bei petroli yafika 3,105 kwa lita

Spread the love

BEI za nishati ya mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa nchini imeongezeka kwa asilimia 11 hadi 21 kuanzia leo Jumatano tarehe 6 Aprili 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Bei hizo mpya zimetangazwa jana Jumanne tarehe 5 Aprili 2022 na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA).

Ikilinganishwa na bei zilizotangazwa tarehe 2 Machi 2022, bei ya rejareja ya mafuta yaliyopitia bandari ya Dar es Salaam imeongezeka kwa Sh 321 kwa lita moja ya petrol sawa na asilimia 12.65, dizeli Sh 289 sawa na asilimia 12.04 na mafuta ya taa Sh 473 sawa na asilimia 21.45.

Bei ya rejareja ya mafuta yaliyopitia bandari ya Tanga yameongeza kwa Sh 285 sawa na asilimia 11.12 kwa lita moja ya petroli na dizeli Sh 295 sawa na asilimia 11.90.

Bei ya rejareja ya mafuta yaliyopitia bandari ya Mtwara ambapo bandari hiyo imepokea mafuta ya dizeli pekee, imeongezeka kwa Sh 281 sawa na asilimia 11.12.

Mabadiliko ya bei hizo yamefanya bei za mafuta aina ya petrol kufikia Sh 2,861 kwa lita hadi Sh 3,105, dizeli Sh 2,692 kwa lita hadi Sh 2,936 na mafuta ya taa kufikia Sh 2,914 hadi Sh 2,925.

Katika taarifa yake kwa umma iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Godfrey Chibulunje, amesema mabadiliko ya bei hizo yamechangiwa na kubadilika kwa bei za mafuta katika soko la dunia, gharama za usafirishaji na thamani ya Shilingi ikilinganishwa na Dola ya kimarekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!