Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Simba vitani tena na wasauzi Robo fainali ya shirikisho Afrika
HabariMichezo

Simba vitani tena na wasauzi Robo fainali ya shirikisho Afrika

Spread the love

 

Klabu ya soka ya Simba Tanzania imepangiwa kukutana na Orlando Pirates ya nchini Afrika kusini katika robo fainali ya kombe la shirikisho barani Afrika mara baada ya kuchezeshwa droo. Anaripoti Damas Ndelema Tudarco (endelea)

Droo hiyo imechezeshwa hii leo tarehe 5 Aprili 2022, jijini Cairo nchini Misri yalipo makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Afrika ‘CAF’

Simba imefika hatua hiyo ya robo fainali baada kufanikiwa kukusanya jumla ya pointi kumi na kumaliza nafasi ya pili katika group D wakiwa na pointi 10, sawa na RS Berkane waliokuwa kwenye nafasi ya kwanza.

Mchezo wa kwanza wa hatua hiyo utapigwa Aprili 17 kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, huku mchezo wa marudiano ukipigwa wiki moja mbeleni tarehe 24 Aprili 2022, Soweto nchini Afrika Kusini.

Hii itakua mara ya pili kwa Simba kupangiwa timu kutoka Afrika Kusini baada ya msimu uliopita kupangiwa kucheza na Kaizer Chief katika hatua kama hii ya robo fainali kwenye michuano ya klabu bigwa na Simba kuondoshwa kwa katika hatua hiyo kwa jumla ya mabao 4-3.

Aidha mshindi kati ya Simba na Oralndo Pirets ata kutana na mshindi war obo fainali ya pili kati ya Al Ahl Tripoli dhidi ya Al ltthad Sc.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!