NI pigo kwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin baada ya Naibu Waziri wa Ulinzi kutoka nchini Belarusi kujiuzulu wadhifa wake kwa kile alichodai kuwa hawezi kumuunga mkono Putin. Anaripoti Mwandishi Wetu.
Naibu Waziri huyo Viktor Gulevich ambaye pia ni Meja Jenerali ameandika barua ya kujiuzulu jana tarehe 6 Machi, 2022 na kuiwasilisha kwa bosi wake yaani Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo, Viktor Khrenin.
Meja Jenerali Gulevich alisema kwamba baadhi ya wanajeshi wa Belarusi walikataa kushiriki katika vita ya Urusi na Ukraine hii ikiwa ni baada ya kupata shinikizo kutoka katika Serikali ya Belarusi kwa sababu tu nchi hiyo ina uhusiano wa karibu na Urusi.
Pamoja na hatua hiyo aliyochukua, Naibu Waziri huyo ni moja ya maofisa wa Serikali ya Belarusi ambaye amewekewa vikwazo na Serikali ya Uingereza kutokana na ukaribu wao na Putin.
Licha ya kusimamia mazoezi ya kijeshi ambayo ni maandalizi ya vikosi vya Jeshi la Belarusi kuungana na wanajeshi wa Urusi, uamuzi wake wa kujiuzulu unakuwa pigo kwa Putin kwani utachochea viongozi wengine wakubwa nchini humo kupinga uamuzi wa Putin kuivamia Ukraine.
Asante mwandishi aliyejiuzuru ni mtu sio serekali pigo liko wapi kwa Putin .mtu kujiuzuru au kufukuzwa kazi ni jambo la kawaida katika ulimwengu wa kazi