Tuesday , 21 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Putin apata pigo, Waziri wa ulinzi ajiuzulu
Kimataifa

Putin apata pigo, Waziri wa ulinzi ajiuzulu

Spread the love

NI pigo kwa Rais wa Urusi, Vladimir Putin baada ya Naibu Waziri wa Ulinzi kutoka nchini Belarusi kujiuzulu wadhifa wake kwa kile alichodai kuwa hawezi kumuunga mkono Putin. Anaripoti Mwandishi Wetu.

Naibu Waziri huyo Viktor Gulevich ambaye pia ni Meja Jenerali ameandika barua ya kujiuzulu jana tarehe 6 Machi, 2022 na kuiwasilisha kwa bosi wake yaani Waziri wa Ulinzi wa nchi hiyo, Viktor Khrenin.

Meja Jenerali Gulevich alisema kwamba baadhi ya wanajeshi wa Belarusi walikataa kushiriki katika vita ya Urusi na Ukraine hii ikiwa ni baada ya kupata shinikizo kutoka katika Serikali ya Belarusi kwa sababu tu nchi hiyo ina uhusiano wa karibu na Urusi.

Pamoja na hatua hiyo aliyochukua, Naibu Waziri huyo ni moja ya maofisa wa Serikali ya Belarusi ambaye amewekewa vikwazo na Serikali ya Uingereza kutokana na ukaribu wao na Putin.

Licha ya kusimamia mazoezi ya kijeshi ambayo ni maandalizi ya vikosi vya Jeshi la Belarusi kuungana na wanajeshi wa Urusi, uamuzi wake wa kujiuzulu unakuwa pigo kwa Putin kwani utachochea viongozi wengine wakubwa nchini humo kupinga uamuzi wa Putin kuivamia Ukraine.

1 Comment

  • Asante mwandishi aliyejiuzuru ni mtu sio serekali pigo liko wapi kwa Putin .mtu kujiuzuru au kufukuzwa kazi ni jambo la kawaida katika ulimwengu wa kazi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaKimataifaTangulizi

Waliowekewa damu yenye VVU, homa ya ini kulipwa fidia trilioni 32.9

Spread the loveWaziri mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak ameahidi kulipa fidia ya...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akwaa kisiki, mahakama yamzuia kuwani urais

Spread the loveMahakama ya katiba nchini Afrika Kusini, katika uamuzi wake imesema...

Habari za SiasaKimataifa

Kiongozi Mkuu Iran amteua mrithi wa Rais Ebrahim

Spread the loveKiongozi wa ngazi ya juu nchini Iran, Ayatollah Ali Khamenei,...

KimataifaTangulizi

Rais Iran afariki kwa ajali ya helkopta

Spread the loveRais wa Iran, Ebrahim Raisi, Waziri wa Mambo ya Nje...

error: Content is protected !!