Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko ZIC yawahakikishia usalama wawekezaji Dubai
Habari Mchanganyiko

ZIC yawahakikishia usalama wawekezaji Dubai

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la (ZIC), Arafat Haji
Spread the love

SHIRIKA la Bima Zanzibar (ZIC) limewakaribisha wawekezaji Visiwani Zanzibar kuwekeza kwa kuwahakikishia usalama wa uwekezaji na mali zao wakati wote wakiwepo Visiwani humo. Anaripoti Matilda Buguye, Zanzibar … (endelea). 

Hayo yameelezwa jana tarehe 25 Februari, 2022 na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la (ZIC), Arafat Haji katika maonesho ya Biashara Kimataifa yanayoendelea katika Falme za Kiarabu-Dubai.

Haji amewakaribisha wadau kuwekeza Visiwani Zanzibar na kupitia Shirika hilo kwani wana uzoefu na masuala ya bima za aina mbalimbali.

“Wawekezaji tunawapa elimu ya namna gani wataweza kuwa na uwekezaji wenye usalama na kuhakikisha kunakua na ajira ya muda mrefu ili kuleta tija na kukuza uchumi na maslahi ya Taifa,” amesema.

Aidha, Haji ameeleza kuwa wawekezaji wanapoamua kushirikisha ZIC wanafanya maamuzi sahihi kwani wapo tayari kuwapa miongozo ya kusimamia uwekezaji huo na kuhakikisha mitaji yao inaleta manufaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

Habari Mchanganyiko

Jeshi la Uhifadhi kujengewa uwezo zaidi

Spread the love  WIZARA ya Maliasili na Utalii imejipanga vyema kuendelea kulijengea...

Habari Mchanganyiko

Wanavyuo Dodoma waonja utamu wa chimbo la nyuki

Spread the love  TAMASHA la Chimbo la Nyuki lililofanyika katika Ukumbi wa...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

error: Content is protected !!