Friday , 17 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa DPP amfutia kesi ya ugaidi kigogo wa ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

DPP amfutia kesi ya ugaidi kigogo wa ACT-Wazalendo

Sylivester Mwakitalu, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP)
Spread the love

 

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Tanga, imemuachia kwa masharti Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ahmed Kidege na wenzake wawili, baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), Sylvester Mwakitalu, kuiomba ifute kesi ya ugaidi iliyokuwa inawakabili mahakamani hapo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Masharti hayo ni, kuwa katika kipindi cha uangalizi wa muda wa miaka mitatu, ambapo Kidege na wenzake watakuwa wanaripoti Polisi kila Jumatatu ya mwanzo wa mwezi.

Taarifa hiyo imetolewa jana tarehe 25 Februari 2022 na Katibu Idara ya Haki za Binadamu na Makundi Maalum, ACT Wazalendo- Taifa, Mbarala Maharagande, muda mfupi baada ya Kidege na wenzake wawili, Ramadhani Songoro na Shaban Mohamed.

“Tarehe 25 Februari, 2022, Mahakama ya Hakimu Mkazi Tanga imefuta kesi ya ugaidi na uhujumu uchumi, iliyokuwa inamkabili dege na wenzake wawili. Hatua hiyo ya mnahakama imetokana na DPP kuwasilisha maombi ya kuifuta kesi hiyo,” imesema taarifa ya Maharagande.

Mbarara Maharagande, Katibu wa Idara ya Haki za Binadamu na Makundi Maalumu ya Chama cha ACT-Wazalendo

Kidege na wenzake walikaa rumande tangu tarehe 24 Septemba 2019.

Akizungumzia hatua hiyo, Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, amesema anaamini hayo masharti ya kuripoti Polisi, aliyopewa Kidege na wenzake, yataondolewa.

“Ni jambo la faraja kwa familia, chama na wapenzi wa haki nchini kuona Kidege na wenzake wameachiwa huru na kesi yao kufutwa baada ya kukaa gerezani kwa zaidi ya miaka miwili. Kwetu sisi, kila mwenzetu anaposhikwa na kufunguliwa kesi, kitu muhimu zaidi kwetu ni uhuru wake,” amesema Ado na kuongeza:

“Kwa namna yoyote ile. Ni matumaini yetu kuwa kupitia jitihada zetu, hata hayo masharti madogo ya kuripoti Polisi mara moja kwa Mwezi yataondolewa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

ACT-Wazalendo yasusia uchaguzi wa ubunge Zanzibar

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo, kimegoma kushiriki uchaguzi mdogo wa Ubunge Jimbo...

error: Content is protected !!