Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wizara ya maji yaingia mkataba na GF Trucks
Habari Mchanganyiko

Wizara ya maji yaingia mkataba na GF Trucks

Spread the love

 

WIZARA ya Maji nchini Tanzania, imeanza mikakati ya kihakikisha inamaliza tatizo la maji mijini na vijijini kwa kuingia mkataba wa kusambaza vifaa vya maji na Kampuni ya GF Trucks & Equipment’s Ltd. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Mkataba huo umesainiwa leo Jumatano, tarehe 9 Februari 2022, jijini Dodoma baina ya Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mhandisi Anthon Sanga na mkurugenzi wa kampuni hiyo, Imran Karmali.

Mhandisi Sanga amewataka walioshinda zabunu hizo za kusambaza vifaa hivyo kuhakikisha wanakamilisha na kukabidhi kwa wakati na isizidi mwezi wa tano ili kuendana na kasi ya Rais Samia Suluhu Hassani ya kuhakikisha miradi inamalizika kwa wakati.

Naye Karmali amesema wao wamelipokea agizo hilo la kukamilisha na kukabidhi vifaa hivyo kwa wakati.

Aidha ameishukuru Serikali kwa kuaminiwa na kwamba wao kama Kampuni hawataingusha katika hilo na ikiwezekana kabla ya mwezi wa tano kila kitu kitakuwa tayari, Ikizingatiwa GF inayomiliki kiwanda cha kutengeneza Magari hapa hapa nchini Tanzani kilichopo Kibaha mkoani Pwani wamejipanga vizuri.

Amesema, kupitia miradi ya maji wao itakuwa kazi nyepesi kwao kwani kupata kwa zabuni hiyo kutaongeza tija katika kiwanda chao na kwa kuwa wana wataalamu wa Kitanzania itakuwa rahisi kukamilisha mahitaji kwa wakati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!