Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko KAGAIGAI: Mifugo 1,257 imekufa Kilimanjaro kwa ukame
Habari Mchanganyiko

KAGAIGAI: Mifugo 1,257 imekufa Kilimanjaro kwa ukame

Spread the love

 

MKUU wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai amesema jumla ya mifugo 1,257 imekufa mkoani humo kwa kukosa maji na malisho kutokana na ukame uliokumba mkoa huo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea). 

Kagaigai ametoa kauli hiyo leo tarehe 22 Januari, 2022 wakati akitoa taarifa ya Mkoa huo kwa Rais Samia Suluhu Hassan ambaye amekwenda kuzindua Tamasha la Utamaduni mkoani humo.

Kagaigai ameitaja mifugo hiyo iliyokufa kuwa ni ng’ombe 841, kondoo 406 na punda 10

Amesema licha ya mafanikio na kazi mbalimbali za maendeleo zinazoendelea, mkoa huo unakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kutonyesha kwa mvua za vuli, hali ambayo imesababisha ukame na vifo vya mifugo.

“Uongozi wa mkoa unaendelea kuchukua hatua mbalimbali ili kukabiliana na hali hiyo. Pamoja na vifo hivyo vya mifugo, hali ya chakula bado ni nzuri, na Mkoa unachakula cha kutosha.

“Pamoja na ukame huo mkoa umejitosheleza kwa chakula hii ni kutokana na kuwa na ziada ya uzalishaji wa chakula tani 40,790 za wanga na tani 10,147 za mikunde zilizopatikana katika msimu nwa mvua 2020/2021.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!