Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia awaomba Kilimanjaro kupunguza matayarisho ya mbege
Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia awaomba Kilimanjaro kupunguza matayarisho ya mbege

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amewaomba wananchi wa mkoa huo kupunguza matayarisho ya kinywaji maarufu mkoani humo cha pombe aina ya mbege, ili kupunguza matumizi ya nafaka. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumamosi tarehe 22 Januari, 2022 katika uwanja wa Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU) wakati akizindua Tamasha la utamaduni mkoa Kilimanjaro, ambalo pia alikuwa mgeni rasmi.

Akitubia wananchi na wageni mbalimbali waliohudhuria tamasha hilo, Rais Samia ambaye pia ni Chifu Hangaya amesema mwaka huu kutakuwa na upungufu wa chakula kidogo.

“Pamoja na kwamba hatukuweza kupanda

mwezi Oktoba lakini tuna akiba ya kutosha ya chakula, niwaombe sana ndugu zangu Kilimanjaro tupunguze kidogo matayarisho ya mbege na vinywaji vingine kwa kutumia nafaka zetu.

“Tujue kwamba mwezi wa 10 hatukupanda, tutapanda mwezi Machi na kutakuwa na upungufu kidogo wa chakula, tutumie chakula tulichonacho ili kije kitufae huko mbele,” amesema Rais Samia.

Aidha, amewaomba Watanzania kuendelea kuomba kwa imani zetu mbalimbali ili Mwenyezi Mungu ajalie mvua yenye neema na baraka.

“Iiendelee kunyesha na kumaliza tatizo la ukame linaloendelea na kuteketeza mifugo na kutuzuia kwenda kwenye kilimo nami Chifu Mkuu nitaendelea kuwa pamoja nanyi katika maombi hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!