Tuesday , 30 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Samia ziarani Misri
Habari Mchanganyiko

Rais Samia ziarani Misri

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan kesho Jumatano tarehe 10 Novemba 2021, ataondoka nchini kwenda Cairo, nchini Misri kwa ziara ya kiserikali ya siku tatu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Ziara hiyo, anaifanya kufuatia mwaliko alioupata kutoka kwa Rais wa Misri, Abdel Fattah Al Sisi.

Taarifa iliyotolewa leo Jumanne, tarehe 9 Novemba 2021 na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu ya Tanzania imesema, katika ziara hiyo, Rais Samia pamoja na mambo mengine atafanya mazungumzo na mwenyeji wake katika maeneo kadhaa ya ushirikiano.

Ushirikiano huo kati ya Tanzania na Misri ikiwemo Nyanja za diplomasia, uchumi, siasa, elimu, utalii na huduma za kijamii.

Haniu amesema, Rais Samian a mwenyeji wake pia, wanatarajia kushuhudia utiaji saini wa mkataba mmoja na hati saba za makubaliano kati ya Tanzania na Misri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Habari Mchanganyiko

TMA yapongezwa kuimarisha ubora na usahihi wa taarifa za Hali ya Hewa

Spread the love  WAFANYAKAZI wa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA),...

error: Content is protected !!