RAIS Samia Suluhu Hassan amesema athari za mabadiliko ya tabianchi hazichagui nchi tajiri wala maskini hivyo kuna umuhimu kwa mataifa yote duniani kuwa na juhudi za pamoja kukabiliana na hali hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).
Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 2 Novemba, 2021 wakati akihutubia mkutano wa Wakuu wa nchi wanaoshiriki mkutano wa 26 kuhusu mabadiliko ya tabianchi unaofanyika huko Glasgow nchini Scotland maarufu kama COP 26.
Katika hotuba hiyo aliyotumia muda wa zaidi ya dakika tatu, Rais Samia ameeleza namna mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri Tanzania katika ardhi ya uzalishaji mali, ongezeko la kina cha bahari, kuyeyuka kwa barafu katika kilele cha Mlima Kilimanjaro na namna ambavyo kisiwa cha Zanzibar kinavyoathirika kwa ongezeko la kiwango cha joto ambalo linaathiri ekolojia inayovutia watalii.
Aidha, ameongeza kuwa athari hizo zinatokea licha ya serikali kuendelea na azma yake ya kutenga hekta milioni 48 kwa ajili ya utunzaji wa misitu.
Rais Samia ameeleza kuwa Tanzania inao mkakati maalumu wa kupambana na mabadiliko ya tabianchi ambao umeainisha hatua kadhaa za kuchukua ikiwamo kupunguza athari za hewa ukaa kwa asilimia kati ya 30 na 35 ifikapo mwaka 2030.
Pia Rais Samia ametoa wito kwa nchi zilizoendelea kuhimiza ahadi zao za kuratibu upatikanaji wa kiasi cha Dola za Marekani bilioni 100 kwa ajili ya kupambana na mabadiliko ya tabianchi hususani kwa nchi zinazoendelea.
Amesema athari zikitokea zitawakumba wote, nchi zilizoendelea kuwa athari zikitokea zitawakumba wote, nchi zilizoendelea na zinazoendelea.
Leave a comment