Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mjane aliyeporwa ardhi na kujengwa kituo cha afya, amvaa RC Songwe
Habari Mchanganyiko

Mjane aliyeporwa ardhi na kujengwa kituo cha afya, amvaa RC Songwe

Kabula Kuba
Spread the love

 

MKAZI wa kata ya Magamba wilayani Songwe mkoani Songwe, Kabula Kuba ambaye pia ni mjane, ameibuka katika Mkutano wa Mkuu wa mkoa huo, Omary Mgumba na kudai Kituo kipya cha afya Magamba kimejengwa katika eneo la ardhi ambayo ni mali ya mumewe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Songwe … (endelea).

Akizungumza katika mkutano huo ambao ni moja ya mikutano ya ziara ya Mkuu huyo wa Mkoa, Kuba amesema eneo la ardhi hiyo palipojengwa kituo hicho limeporwa kwa mumewe bila taarifa.

“Mkuu wa Mkoa mimi ni mjane, nina watoto sita…mmoja ni mlemavu. Hiki Kituo kimejengwa kwenye aneo tulilolimiki mimi na mume wangu ambaye alishafariki. Kimejengwa tena hata bila kunishirikisha, nakuomba unisaidie mjane mimi nipate haki yangu,” alisema Kabula.

Awali kabla ya kutoa uamuzi Mgumba alimkaribisha Diwani wa kata ya Magamba, Kapala Makelele ili atolee ufafanuzi ambapo kwa upande wake diwani huyo alishindwa kutoa maelezo yaliyokamilika hali iliyosababisha wananchi kumzonga kwa kelele na kumtaka aeleze ukweli.

Kutokana na hali hiyo Mkuu huyo wa Mkoa alilazimika kuwauliza wananchi juu ya eneo hilo mmiliki ni nani ambapo kwa pamoja wananchi hao walikiri eneo hilo ni la mjane Kabula.

Aidha, kutokana na majibu hayo, Mgumba aliwaagiza viongozi wa Magamba kukaa chini na mjane huyo ili kuangalia jinsi ya kulimaliza tatizo hilo.

Alisema kituo hicho kimegharimu fedha nyingi zaidi ya milioni 500 hivyo hawezi kubomoa bali busara itumike ili kumaliza mgogoro huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari Mchanganyiko

Shahidi aeleza namna Nathwani alivyomjeruhi jirani yake

Spread the loveMSIMAMIZI wa Msikiti wa Wahindi Lohana aitwae, Ankit Dawda (32)...

error: Content is protected !!