Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia atua K’njaro akitokea Chato
Habari za Siasa

Rais Samia atua K’njaro akitokea Chato

Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo Alhamis, tarehe 14 Oktoba 2021, amewasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kuanzia ziara ya siku tatu mkoani humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Amewasili akitokea Chato, mkoani Kilimanjaro alikoshiriki shughuli ya kilele cha Mbio za Mwenge Maalum wa Uhuru, Kumbukizi ya miaka 22 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere na Wiki ya Vijana.

Mara baada ya kumaliza shughuli hiyo, aliondoka kwenda Kilimanjaro ambapo kwenye uwanja wa ndege, amepokewa na viongozi mbalimbali wa mkoa huo akiwemo Mkuu wa Mkoa, Stephen Kagaigai.

Akiwa mkoani humo, atafanya ziara na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo Barabara ya Bomang’ombe-Sanya Juu-Kamwanga yenye kilomita 98.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

error: Content is protected !!