Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba yashusha kifaa kingine kutoka Senegal
Michezo

Simba yashusha kifaa kingine kutoka Senegal

Spread the love

 

KLABU ya Soka ya Simba imefanikiwa kunasa saini ya mchezaji wa kimataifa wa Senegal Pape Ousmane Sakho (24), kuuelekea msimu mpya wa mashindano. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

 Mchezaji huyo ambaye ni winga wa kushoto ametua ndani ya kikosi cha Simba na kujiunga na timu hiyo nchini Morocco ambapo imeweka kambi kujinoa ka msimu ujao.

Simba ipo katika hatua ya mwisho ya kukamilisha usajili wake, kutokana na kufungwa kwa dirisha hilo kimataifa, kabla ya kaunza kutimua vumbi michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika na Ligi ya Mabingwa.

Usajili huo unafanyika katika kuimalisha kikosi hiko ambacho kimeondokewa na wachezaji wake wawili Clatous Chama pamoja na Luis Miquissone.

Chama ambaye tayari amejiunga na klabu ya Barkane ya nchini Morocco kwa mkataba miaka mitatu.

Kwa upande wa Miquissone huwenda muda wowote kutoka sasa akatangazwa kuwa mchezaji mpya wa mabingwa wa Afrika, klabu ya Al Ahly ya nchini Misri.

Sakho amesajiliwa na klabu ya Simba akitokea Teungueth fc, ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu nchini Senegal.

Mchezaji huyo anakwenda kukamilisha idadi ya wachezaji sita waliosajiliwa na Simba mpaka sasa kuelekea msimu ujao huku watatu wakiwa wazawa.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!