Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo Karia athibitishwa Rais TFF
Michezo

Karia athibitishwa Rais TFF

Wallace Karia, Rais wa TFF
Spread the love

 

WAJUMBE wa mkutano mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), wamemuthibitisha Wallace Karia kuendelea kuwa Rais wa shirikisho hilo kwa muhula wa pili wa miaka minne. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tanga … (endelea).

Karia alikuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo ya urais katika uchaguzi huo, unaofanyika leo Jumamosi, tarehe 7 Agosti 2021, jijini Tanga. Wajumbe hao wamepiga kura ya wazi.

Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi huo, Wakili Kilomoni Kibamba amewahoji wajumbe wa mkutano huo wanaompinga Karia hakuna aliyesimama.

Wakili Kilomoni amesema, wajumbe halali ni 80 ambao wote wamemthibitisha Karia kuendelea kuwa Rais wa TFF sawa na asilimia 100.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!