Sunday , 19 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Elimu bure yaibua tena bungeni, Serikali yatoa majibu
Habari Mchanganyiko

Elimu bure yaibua tena bungeni, Serikali yatoa majibu

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

MBUNGE wa Nkasi Kaskazini (Chadema), Aida Khenani, ameihoji Serikali ya Tanzania, kwa nini wanafunzi wameendelea kuchangishwa michango wakati “inasema elimu ya Shule ya msingi na sekondari ni bure? Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Aida, amehoji hilo, leo Jumatatu, tarehe 7 Juni 2021, bungeni jijini Dodoma, wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

“Je, kwa nini Wazazi wanachangishwa michango ya kuchangia elimu wakati Serikali inasema elimu ya Shule ya Msingi na Sekondari ni bure,” amehoji Aida

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Tamisemi, David Silinde amesema, Serikali kupitia Waraka wa Elimu Namba 5 wa mwaka 2015 iliamua kutoa Elimumsingi bila malipo kuanzia Elimu ya awali hadi Kidato cha Nne.

“Uamuzi huo ulijielekeza katika kutekeleza Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 ambayo ina lengo la kuhakikisha watoto wote wa Kitanzania wenye rika la Elimumsingi wanapata Elimu bila kikwazo chochote ikiwemo Ada au michango,” amesema

Silinde amesema, Serikali ilitoa Waraka wa Elimu Namba 3 wa mwaka 2016 kuhusu utekelezaji wa Elimumsingi Bila Malipo.

“Waraka huu unafafanua maana ya Elimumsingi na kuainisha majukumu ya kila kundi linalohusika katika utoaji wa Elimumsingi bila malipo na kuweka utaratibu wa utekelezaji wake,” amesema

Aida Khenan, Mbunge wa Nkasi Kaskazini (Chadema)

Silinde amesema, majukumu ya jamii na wananchi kuhusu michango yamebainishwa kwenye Waraka wa Elimu Namba 3 wa mwaka 2016.

Amesema, Waraka unaeleza kuwa Kamati za Shule au Bodi za Shule zitashirikisha jamii katika maazimio na maamuzi ya masuala mbalimbali yanayohusu maslahi na maendeleo ya shule hususan uchangiaji wa hiari na kuwasilisha maamuzi hayo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ili kupata kibali.

“Hivyo, uchangiaji katika elimu unaoruhusiwa ni wa hiari na hauhusishi wanafunzi kuzuiwa kuhudhuria masomo,” amesema

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako amesema, kuna michango ya hiari ambayo kupitia kamati za shule, wazazi wana ridhia na kuchangia.

Swali kama hilo la Aida, si la kwanza kuulizwa bungeni, limekuwa likiulizwa mara kwa mara hasa michango inayochangishwa wakati elimu ni bure.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

CCM yamteua Pele kuwa mgombea ubunge Kwahani

Spread the loveKamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Canada yatenga bilioni 38 kutekeleza mradi ya kuinua vijana TZ

Spread the loveSERIKALI ya Canada kupitia ‘CARE International Canada’ imetenga takribani Sh...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Ujenzi kituo cha kupoza umeme Chalinze wafikia asilimia 93.7

Spread the loveKamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeeleza...

Habari Mchanganyiko

Balile ateuliwa rais wa wahariri Afrika Mashariki

Spread the loveJumuiya ya Wahariri wa Afrika Mashariki (EAES), imemchagua Mwenyekiti wa...

error: Content is protected !!