Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali yamjibu Nape kuhusu sakata la korosho
Habari Mchanganyiko

Serikali yamjibu Nape kuhusu sakata la korosho

Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imesema italifanyia kazi ombi la kurejesha fedha za tozo ya mauzo ya nje ya nchi (Exporty Levy), ya zao la korosho, kwa wakulima wa zao hilo, ili waweze kumudu gharama za uzalishaji. Anaripoti Nasra Bakari, DMC…(endelea).

Kauli hiyo ilitolewa jana tarehe 25 Mei 2021, bungeni jijini Dodoma, na Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akimjibu Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nnauye, aliyeomba Serikali irudishe fedha hizo ili kunusuru zao hilo lisife, kutokana na wakulima kushindwa kumudu gharama za uzalishaji.

Akijibu ombi hilo, Bashe alisema ““niwahakikishie kwamba suala la kuingilia na kuharibu mifumo iliyojengwa vizuri hatuwezi kulirudia hilo jambo, lakini suala la export levy nataka niwahakikishie kwenye Bunge hili, kwamba tunalichukua na tunaenda kulifanyia kazi,” alisema Bashe.

Nape Nnauye, Mbunge wa Mtama (CCM)

Aidha, Bashe alisema wizara hiyo inaendelea kuweka mazingira mazuri katika kilimo cha korosho, ili kuongeza uzalishaji wake.

“Jambo jingine ambalo limeongelewa na wabunge kwa uchungu mkubwa, nje ya export levy kwenye zao la korosho ni changamoto ya uzalishaji. Sisi kama Wizara ya Kilimo tunaamini mazao haya ya kilimo yana uwezo kujiendesha yenyewe,” alisema Bashe na kuongeza:

“Na takwimu, tathimini uzoefu umeonesha kwamba wakulima wanaweza kujiendesha wenyewe wakijengewa mazingira mazuri na sisi ndiyo kazi yetu.”

Awali, Nape alisema, tangu Serikali ilipofanya mabadiliko katika sheria ya tasnia ya korosho 2018, ambayo yalisababisha fedha zote za tozo ya mauzo ya zao hilo nje ya nchi, kupelekwa katika mfuko mkuu wa fedha za Serikali, badala ya mfuko wa kuendeleza korosho, uzalishaji wa zao hilo umeshuka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

error: Content is protected !!